Skip to main content

Posts

Showing posts from April 28, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tanzania na Belarus Kuendeleza Ushirikiano

MHESHIMIWA Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameihakikishia Jamhuri ya Belarus kuwa Tanzania itaendeleza ushirikiano na nchini hiyo na kwamba amewaalika wawekezaji na wafanyabiashara kuja nchini  kuangalia fursa za uwekezaji katika sekta za kilimo, uvuvi, elimu na afya. Kauli hiyo imetolewa leo (Jumanne, Aprili 28, 2026) na Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba alipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Belarus, Maxim Ryzhenkov, Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es Salaam. Pia, Dkt. Mwigulu amepokea kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mwaliko wa ziara ya kikazi nchini Belarus wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Belarus, Mheshimiwa Alexander Lukashenko. Waziri Mkuu, amesema Serikali imeboresha mazingira ya uwekezaji na biashara, pia Tanzania kibiashara ipo katika eneo la kimkakati kijiografia kwa kuwa ni kitovu cha Mataifa ya Ukanda wa Afrika Mashariki na ya Kusini mwa Afrika. “Ni kutokana na umuhimu huo, Tanzania kupitia Di...

UMISSETA Nyamagana: Viongozi Wahimiza Amani, Nidhamu na Uadilifu

  ​Kutoka: Dawati la Habari Polisi Mwanza Viongozi wa Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza wamewataka wanafunzi wanaoshiriki Mashindano ya Michezo kwa Shule za Sekondari (UMISSETA) ngazi ya wilaya, kuzingatia nidhamu, amani na uadilifu ili kupata wawakilishi bora watakaotetea ubingwa wa mkoa na taifa. Wito huo umetolewa Aprili 27, 2026, wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Nsumba. ​Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Amina Makilagi, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Thomas Salala, aliwahimiza wasimamizi wa mashindano hayo kutenda haki wakati wa uteuzi wa washiriki. Alisisitiza kuwa ni muhimu kupata vipaji halisi vitakavyoiwezesha Nyamagana na Mkoa wa Mwanza kuendelea kushikilia nafasi za juu katika ngazi ya mkoa na kitaifa.  Sambamba na hilo, Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Nyamagana, SSP Virginia Sodoka, aliwataka wanafunzi na washiriki wote kudumisha amani na utulivu muda wote wa mashindano hayo ili kufikia malengo ...

Waziri Katambi Atoa Maagizo Mazito Wizara ya Mambo ya Ndani

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi ameitaka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuzingatia mambo 10 vya msingi huku akisisitiza nidhamu, haki, weledi na uadilifu katika utekelezaji wa majukumu na wajibu wa wizara wa kulinda raia na mali zao. Ametoa maagizo hayo wakati akifungua Kikao cha Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ambacho kimefanyika leo,jijini Dodoma ambapo kilihudhuriwa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Ally Senga Gugu,Wakuu wa Idara na Vitengo wa wizara,Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Katungu, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, CGF John Masunga, Kamishna wa Fedha na Lojistiki wa Jeshi la Polisi, CP Liberatus Sabas, Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, CP Kombo Khamis Kombo,Wawakilishi wa Idara ya Uhamiaji, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA) na wawakilishi wa watumishi wa wizara. “Naomba tuzingatie yafuatayo; Moja, kusimamia na kuhakikisha mpango mkakati, mipango dira, dhima na majukumu ya wizara y...

REA Yatoa Elimu ya Nishati Safi kwa Wananchi Tamasha la Kilimo Iwambi Mbeya.*

  📍 *Iwambi,Mbeya*  Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeendelea kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi kwa wananchi katika Tamasha la Kilimo linalofanyika katika viwanja vya Iwambi, mkoani Mbeya. Akizungumza wakati wa tamasha hilo, Mhandisi wa Miradi kutoka REA, Ramadhani Mganga, amesema kuwa lengo la ushiriki wao ni kuwahamasisha wananchi kutumia nishati safi na salama kwa kupikia ili kulinda afya zao na mazingira. Ameeleza kuwa REA inaendelea kusambaza na kuhamasisha matumizi ya teknolojia mbalimbali za nishati safi ikiwemo majiko ya umeme, majiko ya gesi pamoja na majiko banifu, ambayo yanasaidia kupunguza matumizi ya kuni na mkaa. “Ni muhimu kwa wananchi kuelewa faida za nishati safi, si tu katika kulinda mazingira bali pia katika kuboresha afya kwa kupunguza athari za moshi unaotokana na nishati zisizo salama,” amesema Mganga. Aidha, amebainisha kuwa kupitia miradi mbalimbali inayoendelea, upatikanaji wa umeme vijijini umeimarika kwa kiwango kikubwa, hatua inayowezesha ...

Dampo la Pugu Likitumika Vizuri Litazalisha Mbolea Hai-Chongolo

WAZIRI wa Kilimo, Daniel Chongolo, amewasilisha Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka 2026/2027 leo Aprili 28, 2026, Bungeni jijini Dodoma ambapo amesema ni wakati kwa wawekezaji nchini kutumia fursa ya taka ozo kuzalisha mbolea hai, hatua itakayosaidia kuongeza tija kwenye kilimo sambamba na kulinda mazingira. Akiwasilisha bajeti ya wizara yake Bungeni jijini Dodoma leo  April 28,2026 Bungeni Jijini Dodoma, Waziri wa Kilimo Mhe. Daniel Chongolo amezitaka  halmashauri zote nchini  kuiga mifano iliyopo kwa kuwekeza kwenye viwanda vya kutengeneza mbolea hai kutokana na wingi wa taka zinazozalishwa. "Ninatoa rai kwa Halmashauri nchini kuiga kuwekeza kwenye viwanda vya kutengeneza mbolea hai kwa kutumia fursa ya taka ozo ambazo zinapatikana kwa wingi katika maeneo yao ikiwa na lengo pia la kusafisha na kutunza mazingira". Amesisitiza  "Kwa mfano Jiji la Dar Es Salaam kwenye dampo la Pugu, kwanza itasaidia kupunguza taka na kuzalisha mbol...

Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Samia Aongoza Kikao cha Kamati Kuu

 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiongoza Kikao cha siku mbili cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM kinachokutana jijini Dar Es Salaam , leo Jumanne tarehe 28 Aprili 2026.