Na Hamida Ramadhan- Dodoma Foundation For Disabilities Hope, (FDH)taasisi isiyokuwa ya kiserikali, imepata ufadhili wa shilingi milioni 40 kwa ajili ya mradi wa kuwawezesha watu wenye ulemavu katika masuala ya uongozi na kukuza demokrasia. Ufadhili huo umetolewa na shirika la Abilis Foundation yenye ofisi zake nchini Tanzania, mkoani Arusha. Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Foundation For Disabilities Hope, Michael Salali, alisema mradi huo unalenga kuwafikia watu 300 wenye ulemavu katika wilaya ya Kondoa. “Tunaimani mradi huu umekuja kwa wakati muafaka, hasa baada ya uchaguzi mdogo na kuelekea uchaguzi mkuu. "Tunataka kuwajengea uwezo watu wenye ulemavu kujitokeza kuchagua na kugombea nafasi mbalimbali za uongozi bila kujihisi wanyonge,” alisema Salali. Hata hivyo Tasisi hiyo imeishukuru Abilis Foundation kwa kufanikisha mradi huo muhimu. Kwa upande wake Furaha William, Afisa Habari wa taasisi hiyo, alieleza kuwa mradi huo pia unalenga wanawake na was...