Aliyekuwa waziri mkuu nchini Kenya Raila Odinga amefariki akiwa na umri wa miaka 80. Raila amefariki wakati akifanyiwa matibabu katika hospitali moja nchini India. Rais wa Kenya William Ruto ametangaza siku saba za maombolezo ya kitaifa kufuatia kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga. Katika hotuba yake kwa taifa kupitia televisheni, Rais Ruto alimtaja Odinga kama "mzalendo mwenye ujasiri usio wa kawaida." Alisema bendera ya taifa itapepea nusu mlingoti kote nchini Kenya na katika balozi zote za Kenya nje ya nchi. Kama ishara ya heshima, nimeahirisha shughuli zangu zote za umma kwa siku zijazo, na ninawaomba wafanyikazi wengine wote wa umma na viongozi kufanya vivyo hivyo ili tujiunge na taifa katika kipindi hiki cha maombolezo," Ruto alisema. Rais Ruto pia ametangaza kuwa Odinga ataandaliwa mazishi ya kitaifa kwa heshima kamili. Aliongeza kuwa serikali ya India, ambapo waziri mkuu huyo wa zamani alifariki alipokuwa akipokea matibabu, imejitolea kuwezesha kurejeshwa...
Marato tv - Sauti ya Jamii