Skip to main content

Posts

Showing posts from May 15, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Sillo Aunga Mkono Vipaji vya Michezo Babati Vijijini

Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Daniel Sillo ametoa tracksuit 25 za mazoezi kwa wanafunzi mbalimbali wa shule za msingi waliopo kwenye kambi ya maandalizi ya mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) ngazi ya mkoa na baadaye taifa. Kambi hiyo ya maandalizi imewekwa katika Shule ya Msingi Dareda kati wilayani Babati, ambapo wanafunzi hao wanaendelea kujifua kwa ajili ya kuiwakilisha Halmashauri ya Wilaya ya Babati katika mashindano hayo muhimu ya michezo na sanaa. Tracksuit hizo zimekabidhiwa kwa niaba ya mbunge huyo na Katibu wa Mbunge, Waziri Juma, ambaye amewatakia kila la heri wanafunzi hao wanapojiandaa kwenda kushindana na wenzao kutoka halmashauri mbalimbali za mkoa na taifa. Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Waziri Juma amesema Mheshimiwa Sillo anaendelea kuthamini michezo kama sehemu muhimu ya kukuza vipaji vya watoto, kuimarisha afya pamoja na kujenga nid...

Dereva wa Bodaboda Auawa Morogoro

Dereva bodaboda aliyefahamika kwa jina la Ally Kambi (24), mkazi wa Kingolwira Manispaa ya Morogoro, anadaiwa kuuawa na watu wasiojulikana baada ya kukodi huduma yake ya usafiri, kisha kuporwa pikipiki yake. Tukio hilo linasadikika lilitokea katika eneo la Mkambarani Wilaya ya Morogoro, ambapo mwili wa marehemu ulipatikana porini ukiwa na majeraha. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Andrew Kantimbo, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi ili kuwabaini waliohusika na mauaji hayo. Akizungumzia tukio hilo na Moja ya chomba Cha Habari baba mkubwa wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Shukuru Msonga amesema Ally aliondoka Mei 11, 2026 majira ya usiku baada ya kukodiwa na mtu asiyejulikana, lakini hakurejea nyumbani. Msonga amesema baada ya kijana huyo kutorejea kwa siku nzima, familia ilitoa taarifa kwa Serikali ya mtaa na kituo cha polisi, ambapo juhudi za kumtafuta zilianza mara moja. “Tulihangaika kumtafuta maeneo mbalimbali, tulifika...

Waziri Mkuu Akutana na Wabunge wa Mikoa ya Mwanza, Mara na Simiyu

_▪️Wajadili mipango endelevu ya ujenzi wa miundombinu_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amekutana na kufanya kikao kazi na wabunge wa mikoa ya Mwanza, Mara na Simiyu pamoja na viongozi kutoka Wizara ya Uchukuzi, Wizara ya Ujenzi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI pamoja na Wizara ya Fedha. Lengo la kikao hicho lilikuwa ni kujadili maendeleo ya miradi ya kimkakati ya miundombinu katika mikoa hiyo hususan ukamilishaji wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwanza pamoja na viwanja vya ndege vya Serengeti na Musoma. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Spika, Bungeni jijini Dodoma, leo Ijumaa Mei 15, 2026, pia kilihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza pamoja na wakuu wa taasisi za usafirishaji na miundombinu ikiwemo reli, barabara na viwanja vya ndege pamoja na wataalamu mbalimbali kutoka Serikalini.

Tanzania Pushes for People-Centered Tech Diplomacy at Geneva AI Governance Meeting

By Prosper Makene Tanzania used its participation in the International Telecommunication Union’s two-day high-level meeting on AI Governance in Geneva to reaffirm its commitment to technology policy that delivers direct benefits to citizens. Minister of Communication and Information Technology and MP for Kibamba, Hon. Angellah Jasmine Kairuki, represented Tanzania at the meeting. Hon. Kairuki also serves as Vice Chair of the Executive Committee of the Global Initiative on AI and Virtual Worlds established by the ITU. She said the country is ready to engage and ensure that global discussions on artificial intelligence translate into practical gains at home. The forum brought together governments, industry, and civil society to shape international norms on the safe and equitable use of AI. While in Geneva, the Minister visited the offices of the Permanent Mission of Tanzania to the UN. She met with staff and stressed that Tanzania must remain at the forefront of multilateral engagements,...

Funguni Sekondari Yazidi Kuwajengea Uwezo Wanafunzi Kujiajiri Baada ya Kuhitimu Masomo Yao

NA: MWANDISHI WETU, PANGANI Suala la kuwajenga wanafunzi kuwa mahiri katika stadi na ujuzi mbalimbali ndiyo mwelekeo wa Taifa letu katika kuwaandaa wahitimu wenye uwezo wa kuhimili ushindani wa kiuchumi.  Katika Shule ya Sekondari Funguni ya wilayani Pangani mkoani Tanga, mkazo huo unaendelezwa kwa kasi hasa katika somo la Biashara (Business Studies) ambapo baada ya kusoma kwa nadharia, wanafunzi hufanyia kazi walichojifunza kwa vitendo ili kuwajenga katika kujitegemea. Katika maboresho ya mtaala yaliyofanywa na serikalia ni pamoja na kuwajengea uwezo wanafunzi kuweza kuanzisha shughuli zao binafsi za kuwaingizia kipato ili wajitegemee hasa baada ya kuhitimu masomo yao. Mwalimu Shija Clement anayefundisha somo la Biashara Funguni Sekondari, anasimamia kikamilifu ujifunzaji huo kwa vitendo.  Mathalani, Mei 15, 2026, amesimamia uandaaji wa vitafunwa kwa mara ya pili, kwa wanafunzi wa kidato cha pili ikiwa ni mwendelezo wa utaratibu wa kuwajengea uwezo wanafunzi kubuni, kuanzisha...

Tanzania Yaendelea Kung’ara Duniani Katika Sekta ya Utalii, Yashika Nafasi ya 6 Afrika na Mashariki ya Kati

TANZANIA imeendelea kufanya vizuri katika sekta ya utalii duniani, ambapo imefanikiwa kushika nafasi ya 6 katika ukanda wa Afrika na Mashariki ya Kati kwa ukuaji wa watalii wa kimataifa, huku pia ikiorodheshwa nafasi ya tatu duniani kwa masoko ya utalii yaliyofanya vizuri zaidi kwa matumizi ya watalii mwaka 2025 ukilinganisha na mwaka 2024. Akieleza mafanikio hayo Bungeni Jijini Dodoma wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, amesema hatua hiyo ni uthibitisho wa mafanikio ya sera na mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kukuza sekta ya utalii nchini. Amefafanua kuwa mafanikio hayo yametokana na maboresho ya miundombinu ya utalii, uimarishaji wa vivutio vya asili, kuimarika kwa huduma kwa wageni, pamoja na kampeni za kimkakati za kuitangaza Tanzania katika masoko ya kimataifa. Waziri Kijaji amesisitiza kuwa mwitikio mkubwa wa watalii na ongezeko la matumizi yao nchini ni ishara ya ...

Tanzania Kunufaika na Miss World 2027 Kutangaza Utalii Duniani

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, ameliambia Bunge jijini Dodoma Mei 15, 2026 kuwa Tanzania imejipanga kikamilifu kutumia fursa ya Shindano la 74 la Ulimbwende wa Dunia (Miss World 2027) katika kuimarisha na kutangaza sekta ya utalii kimataifa. Akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Kijaji amesema mashindano hayo makubwa duniani, yatakayofanyika Mei 2027 nchini Tanzania, yanatarajiwa kuvutia washiriki 120 kutoka mataifa mbalimbali pamoja na wageni takriban 20,000, hatua itakayolifanya taifa kuwa kitovu cha macho ya dunia. Ameeleza kuwa tukio hilo ni fursa muhimu ya kipekee kwa Tanzania kujitangaza kimataifa kupitia vivutio vyake vya utalii, utamaduni na urithi wa asili, hivyo kuongeza mapato na idadi ya watalii wanaotembelea nchi. Katika maandalizi hayo, Wizara kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) itawahamasisha wadau wa sekta ya utalii kuandaa na kuuza vifurushi vya safari kupitia majukwaa ya kidijitali ya TTB (booking platforms). Samb...

Afcon 2027 Kufungua Fursa Mpya Utalii Tanzania

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji amesema Serikali imejipanga kutumia Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 kuitangaza Tanzania kimataifa na kuongeza mchango wa sekta ya utalii katika uchumi wa taifa kupitia maboresho ya miundombinu, matangazo ya kimataifa na vifurushi maalum vya utalii. Dkt. Kijaji amesema Tanzania ambayo ni miongoni mwa nchi tatu za Afrika Mashariki zitakazoandaa AFCON 2027, itanufaika kwa kiasi kikubwa kutokana na mashindano hayo yanayotarajiwa kuvutia watazamaji wa viwanjani milioni 1.8 pamoja na watazamaji wa televisheni bilioni 1.9 duniani kote. Akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2026/2027 leo Mei 15, 2026 Bungeni jijini Dodoma, amesema Wizara imeandaa mkakati maalum wa kuitangaza Tanzania kabla, wakati na baada ya mashindano hayo. Amesema kabla ya AFCON 2027, Tanzania itaanza kujitangaza katika Mashindano ya Kombe la Dunia 2026 yatakayofanyika nchini Marekani kupitia mabango ya kidijitali pamoj...