📍 Aishukuru Kamati Kuu ya Halmashauri ya Kuu ya CCM Taifa kwa kumteua kuwa mgombea Na Mwandishi Wetu, Korogwe MGOMBEA wa kiti cha ubunge Jimbo la Korogwe Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), CPA Charles Njama amesema dhamana aliyopewa kupeperusha bendera ya chama hicho kwenye kinyang'anyiro cha ubunge, ni deni kubwa kwake la kuleta maendeleo mjini Korogwe. Akizungumza tarehe 26/8 katika ofisi za chama hicho zilizopo eneo la Majengo mjini hapa mara baada ya kukabidhiwa fomu ya kugombea ubunge na msimamizi wa uchaguzi Elinlaa Kivaya, Njama alisema anaishukuru Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM kwa kumuamini na kurejesha jina lake ili agombee ubunge katika Jimbo hilo. "Naishukuru Kamati Kuu, Kamati ya Siasa mkoa, Kamati ya Siasa wilaya na wajumbe walionichagua, kwa kujenga imani na Mimi kati ya wenzangu Saba kupeperusha bendera ya chama, Mimi siyo mshindi kilichoshinda ni chama," alisema. Njama alisema imani aliyopewa na chama ni deni kubwa ambalo lipo moyoni m...
Marato tv - Sauti ya Jamii