Skip to main content

Posts

Showing posts from October 30, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali ipo tayari kupokea mapendekezo ya kufanikisha mpango wa bima ya afya kwa wote

Serikali imewahakikishia wananchi kuwa ina dhamira ya dhati ya kutekeleza mpango wa bima ya afya kwa wote, na kutoa wito kwa washiriki wa kongamano la mpango wa bima ya afya kwa wote na mdahalo wa kitaifa kuhusu ufadhili wa sekta ya afya kuja na mapendekezo yatakayosaidia kutimiza dhamira hiyo. Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) wakati anafungua matukio hayo mawili yanayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha jijini Arusha Oktoba 30, 2024. Matukio hayo yanayofanyika kwa siku nne hadi Novemba 1, 2024 yamekusanya wadau wa afya kutoka ndani na nje ya nchi ili kwa pamoja kujadili mikakati na mbinu bora zitakazoiwezesha Serikali kuwa na mipango endelevu ya kuhakikisha kuwa kila mwananchi, anakuwa na bima ya afya itakayomwezesha kupata matibabu bila kuangalia kipato chake. Waziri Mkuu ambaye aliambatana na viongozi mbalimbali katika hafla hiyo ya ufunguzi, wakiwemo Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama (Mb),...

Mbunge Mavunde awapa Tabasamu watu wenye ulemavu

▪️Agawa viti mwendo 20 kwa wanafunzi na wenye ulemavu ▪️Mbunge Keisha apongeza juhudi za Mbunge Mavunde kwa watu wenye ulemavu 𝐃𝐨𝐝𝐨𝐦𝐚 Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh. Anthony Mavunde amegawa vitu mwendo 20 kwa wanafunzi na wananchi wenye ulemavu Jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya utatuzi wa changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu Jijini Dodoma. “Imekuwa ni utamaduni wangu kila mwaka kusaidia makundi yenye mahitaji maalum juu ya upatikanaji wa vifaa saidizi ikiwemo viti mwendo. Leo nipo hapa kukabidhi viti 20 ambavyo wadau wa maendeleo wametuunga mkono kwa ajili ya wanaDodoma na hasa wanafunzi ambao wamekuwa wakipata wakati mgumu kutokana na ukosefu wa viti mwendo”Alisema Mavunde Naye Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu(SHIVYAWATA)Dodoma Ndg. Hassan Lubuva amemshukuru Mbunge Mavunde kwa kuwa karibu na watu wenye ulemavu wa Dodoma na kutoa rai kwa mashirika na watu binafsi kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu. Akizungumza katika m...

Biteko kumwakilisha Rais Samia kuaga mwili wa mkuu wa majeshi mstaafu

NAIBU Waziri Mkuu na waziri wa Nishati Mh Dkt Dotto Biteko kuongoza Maafisa Jenerali,  Maafisa Wakuu, Maafisa wadogo na Askari wa JWTZ kuaga mwili wa mkuu wa majeshi mstaafu Jenerali David Bugozi Musuguri. Mh Biteko atamwakilisha amiri jeshi mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania mh Dkt Samia Suluhu Hassan kuaga mwili huo novemba 01- 2024 katika hospitali kuu ya Jeshi Lugalo Jijini Dar es Salaam.  Zoezi hilo linatarajiwa kufanyika saa tatu asubuhi kabla ya mwili huo kusafirishwa kuelekea Butiama mkoani Mara kwa ajili ya shughuli ya mazishi. Jenerali Musuguri alifariki dunia asubuhi ya Oktoba 29 mwaka 2024 wakati akapatiwa matibabu hospitali ya Kanda ya Bugando jijini Mwanza,enzi za uhai wake ameshika nafasi mbalimbali ndani ya jeshi hadi kuwa mkuu wa majeshi kuanzia mwaka 1980 hadi 1988 alipostaafu kwa heshima. Jenerali Musuguri akiwa jeshini amekuwa mkufunzi wa askari wakati wa ukoloni wa Mwingereza. Mwaka 1953 alimfundisha pia Idd Amin katika kambi ya mafunzo ya Kahawa...

Serikali imetangaza kushirikisha wadau katika mpango wa bima ya afya kwa wote

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa Washirika wa Maendeleo kushikiriana na Serikali katika kufanikisha utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote na kusaidia kuimarisha mfumo wa ugharamiaji huduma za afya ili kuufanya kuwa endelevu. Mheshimiwa Majaliwa amesema ili kuimarisha mfumo wa ugharimiaji wa huduma za afya Serikali tayari imeanza kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kuendelea kuongeza kiwango cha bajeti ya Sekta ya Afya. Ametoa wito huo leo (Jumatano Oktoba 30, 2024) alipomwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi wa mdahalo wa Bima ya Afya kwa Wote na Jukwaa la Kitaifa la Ugharamiaji wa Huduma za Afya kwa ajili ya utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote (Universal Health Insurance - UHI), jijini Arusha. “Pia, tumeanzisha mfuko kwa ajili ya kugharimia wananchi wasio na uwezo, tumebainisha vyanzo mahsusi vya fedha kwa ajili ya kugharimia Bima ya Afya kwa wananchi wasio na uwezo ambapo katika bajeti ya mwaka 2024/2025 zimetengwa shilingi bi...

Mwita amuua Daniel kwa wivu wa kimapenzi

Jeshi la polisi mkoani mwanza linamshikilia Amos Mwita Mkazi wa Bugarika bendera tatu,wilayani nyamagana kwa tuhuma za mauaji ya Daniel Kisire Mkazi wa bugarika sokoni. Kamanda wa polisi mkoa wa mwanza Wilbroad Mutafungwa amesema kuwa Mwita anatuhumiwa kutenda mauaji hayo kwa kumchoma Kisire na Kitu chenye ncha kali shingoni baada ya kuzuka kwa ugomvi uliozuka uliotokana na wivu wa kimapenzi na kusababisha kifo chake. Kamanda Mutafungwa amesema kuwa mara ya baada ya mtuhumiwa Mwita kufanya tukio hilo alitoroka na kwenda kusikojulikana ambapo Jeshi la polisi lilifanikiwa kumtia mbaroni akiwa mafichoni nyumbani kwa rafiki yake katika eneo la bugarika. "Daniel Kisire ambaye ni marehemu na Amos Mwita ambaye ni mtuhumiwa walikuwa wanaishi Jirani katika eneo la bugarika ambapo marehemu alimtaka kimapenzi binti mmoja ambaye alimkatalia na baadaye binti huyo alianza mahusiano na Mwita na huo ndo ukawa chanzo cha ugomvi baina ya marehemu na mtuhumiwa"alisema kamanda mutafungwa Mtuhumi...

Rhobi Samwelly Awataka Wanafunzi wa Kike Chief Ihunyo Sekondari Kujitambua

  Na Fresha Kinasa. MKURUGENZI wa Shirika la Hope for Girls and Women in Tanzania (HGWT) Rhobi Samwelly   amewataka wanafunzi wa kike wanaosoma kidato cha tano na  kidato cha sita Katika Sekondari  ya Wasichana  ya  Chief Ihunyo iliyopo Wilayani Butiama Mkoani Mara kusoma kwa bidii, kujisimamia na  kujitambua ili  watimize ndoto zao.  Rhobi ambaye  amekuwa akijishughulisha na kutetea haki za wanawake na watoto kupitia Shirika analoliongoza, ameyasema hayo Octoba 30, 2024,  wakati akizungumza na Wanafunzi hao (580) shuleni hapo.  Ambapo pia,  ametoa elimu ya madhara ya  ukatili wa Kijinsia.  Rhobi amesema kuwa, Taifa na Jamii inahitaji Wasomi wenye ujuzi na utaalamu  watakaosaidia kuendelea kuleta mageuzi chanya katika nyanja mbalimbali. Hivyo  amewahimiza  kutumia fursa waliyonayo kwa sasa kusoma kwa bidii na kuweka nidhamu mbele  kufikia malengo yao kwa ufanisi.   Ametolea mfan...

Dereva wa basi lililosababisha ajali iliyosababisha vifo vya watu wanane apandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka 64

Na Dawati la Polisi Mwanza Dereva wa basi la Ahsante Rabi Shedrack Swai (37) anayetuhumiwa kusababisha ajali Oktoba 22.2024 eneo la Ukirigulu, wilaya ya Misungwi, mkoani Mwanza amepandishwa kizimbani Oktoba 29,2025 katika mahakama ya wilaya ya Misungwi na kusomewa mashtaka 64 ikiwemo kuendesha gari kwa uzembe katika Barabara ya Umma, kusababisha vifo, majeruhi, uharibifu wa miundombinu na mali. Akisoma mashtaka hayo katika kesi ya Trafiki namba 30855/2024, linalomkabili dereva huyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Wilaya ya Misungwi, Esther Marick,  Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Ramson Salehe akisaidiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Lilian Meli alisema mshtakiwa alitenda makosa hayo  kinyume na Kifungu cha 41, 63 (2) (b) na 27 (1) cha Sheria ya Usalama Barabarani namba 168 marejeo ya mwaka 2002. Salehe ameieleza mahakama hiyo kuwa mshtakiwa  anashtakiwa kwa makosa 64 yakiwemo ya kuendesha gari kwa uzembe katika barabara ya umma  na kusababisha vifo vy...

Waziri mkuu kufungua kongamano la bima ya afya kwa wote

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Oktoba 30, 2024 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi wa mdahalo wa Bima ya Afya kwa Wote na Jukwaa la Kitaifa la Ugharamiaji wa Huduma za Afya kwa ajili ya utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote (Universal Health Insurance - UHI) Kongamano hilo linalofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Arusha, limelenga kuwashirikisha wadau wote muhimu kuweka mikakati madhubuti ya utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote. Kaulimbiu ya Kongamano hilo ni “_Ugharimiaji endelevu wa huduma za afya nchini: Kuimarisha mfumo wa Bima ya Afya ili kufikia afya kwa wote 2030_”