Arusha, Novemba 27, 2025 Sekta ya madini inaendelea kunufaika na mageuzi ya kidijitali, baada ya mfumo wa mnada wa madini ya vito kupitia Soko la Bidhaa Tanzania (TMX) kuonyesha matokeo chanya katika kuongeza uwazi, ushindani na kudhibiti utoroshaji wa madini nchini. Akizungumza katika mnada wa tatu wa madini ya vito uliofanyika katika Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC), Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini kutoka Tume ya Madini, CPA Venance Kasiki, amesema mfumo huo umeleta mapinduzi katika namna wafanyabiashara wanavyonunua madini. Kasiki amesema kupitia TMX, ununuzi unafanyika kwa njia ya kidijitali na kwa uwazi mkubwa ambapo washiriki wote wanaona hatua kwa hatua mwenendo wa bei, hatua inayotofautiana na utaratibu wa zamani wa matumizi ya bahasha ambao haukuwa na uwazi wa kutosha. Ameeleza kuwa mageuzi hayo yameongeza hamasa kwa wafanyabiashara kushiriki kwa wingi katika minada, huku Serikali ikipata mapato halali na wauzaji wakipata bei stahiki. “Mfumo huu unaimarisha uwazi...
Marato tv - Sauti ya Jamii