Skip to main content

Posts

Showing posts from May 12, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Halmashauri zatakiwa Kusimamia zoezi la Usafi wa Barabara

Iringa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Raisi-Tamisemi anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila amezitaka halmashauri zote nchini kuhakikisha zinasimamia kikamilifu zoezi la usafi wa barabara, akisisitiza kuwa serikali imewekeza fedha nyingi katika ujenzi wa miundombinu hiyo muhimu. Mhandisi Mativila amesema hayo mkoani  Iringa wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya Wenda–Mgama Km.19 inayojengwa na TARURA kupitia mradi wa RISE kwa gharama ya shilingi bilioni 29.7 ambayo imefikia asilimia 99 ya utekelezaji. Mhandisi Mativila amesema usimamizi mzuri wa barabara unahitajika ili kuhakikisha barabara hizo zinadumu na kuleta manufaa yaliyokusudiwa kwa wananchi. "Ni wajibu wa kila halmashauri kuhakikisha kuwa barabara hizi zinatunzwa, hasa kwa kuhakikisha zinaendelea kuwa safi na salama kwa matumizi. Hili ni jukumu la pamoja,” amesema Mativila. Ameongeza kuwa uwepo wa barabara bora unachochea shughuli za kiuchumi na kijamii kwa kuwawezesha wananchi kusafirisha bidhaa na hudu...

Simba Logistics wampongeza Rais upanuzi bandari ya Tanga

Na Mashaka Mhando, Tanga KUFUATIA kuboreshwa kwa bandari ya Tanga,  Kampuni ya Simba Logistics ya Jijini Dar es Salaam, wamemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kufanya maboresho hayo ambayo yamesaidia kampuni hiyo kuajiri vijana 300. Akizungumza katika sherehe za siku ya mazingira zilizofanyika katika shule ya sekondari Ummy Mwalimu iliyopo kata ya Maweni, Meneja Utekelezaji wa Simba Logistics Daud Kanuti alisema wanaishukuru serikali kupanua bandari hiyo ambayo imeanza kuleta manufaa. "Mheshimiwa mkuu wa mkoa tunaomba utufikishie salamu zetu kwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa maboresho aliyofanya bandari ya Tanga, imesaidia kuongoza ajira, vijana 300 wa Kitanga tumewapa ajira ya muda mrefu na muda mfupi, tunaishukuru sana serikali," alisema. Kanuti alisema kuwa kampuni hiyo iliyoanza kazi katika Jiji la Tanga mwaka 2019 baada ya maboresho hayo, tayari wameleta meli 10 ambazo zimekuja na bidhaa mbalimbali. Kuhusu suala la mazingira Kanuti alisema kampuni hiyo inaunga ...

Serikali inaithamini Sekta Binafsi - Waziri Mkuu

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazofanya kazi Serikali inaithamini Sekta Binafsi - Waziri Mkuu karibu sana na sekta binafsi ili kukuza uchumi na kuleta maendeleo kwa wananchi wake. Ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumatatu, Mei 12, 2025) wakati akishiriki mjadala uliojumuisha mawaziri Serikali inaithamini Sekta Binafsi - Waziri Mkuu inaithamini Sekta Binafsi - Waziri Mkuu wanne kutoka Tanzania, Ivory Coast, Guinea na Cameroun katika moja ya vikao vya jukwaa la siku mbili la Maafisa Watendaji Wakuu barani Afrika ambao unaendelea hoteli ya Sofitel jijini Abidjan, Ivory Coast. Waziri Mkuu Majaliwa ambaye anamwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika jukwaa hilo alitumia fursa hiyo kuelezea namna ambavyo Serikali ya Tanzania imekuwa ikiishirikisha sekta binafsi kwa kufungua milango ya fursa mbalimbali ili iweze kutumika na kuleta manufaa katika nchi. “Serikali ya Tanzania inafanya kazi kwa karibu na Tanzania Private Sector Foundation, ...

Kamishna Kuji Awaapisha Makamishna Wapya wa Uhifadhi Tanapa

Na Philipo Hassan - Arusha.  Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Musa Nassoro Kuji leo Mei, 12, 2025 amewaapisha na kuwavisha vyeo Makamishna Wasaidizi wa Uhifadhi Tisa (9) ili kuboresha utendaji kazi wa Shirika zoezi ambalo limefanyika katika Ofisi za TANAPA Makao Makuu jijini, Arusha. Akizungumza katika hafla hiyo Kamishna Kuji, alitoa msisitizo kwa Makamishna hao kufanya Kazi kwa bidii, weledi na kusikiliza watu wanaowaongoza ili kuleta tija zaidi  pamoja na kufikia malengo ya Shirika na Taifa kwa ujumla. “Nendeni mkachape kazi kwa bidii na weledi huku mkiishi viapo vyenu mlivyoapa leo. Kiongozi mzuri ni yule anaesikiliza mawazo ya watu wake anaowaongoza hivyo, mkasikilize watu mnaowaongoza” alisisitiza Kamishna Kuji. Akitoa shukurani kwa niaba ya Makamisha wapya, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Simon Aweda ambaye ndiye Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Burigi-Chato alishukuru Bodi ya Wadhamini TANAPA pamoja na Uongozi wa Shirika kwa kutambua juhudi...

Ng'wasi Kamani amwakilisha Wanu katika Kongamano la vijana

   Ateta na mabinti wa mkoa wa wa kusini Unguja Amwakilisha Mhe Wanu Hafidh Ameir (Mb) kwenye kongamano la Binti na Uongozi.  Mbunge wa Viti Maalum kundi la Vijana Taifa Mhe Ng'wasi Kamani amepata nafasi ya kushiriki kama Mgeni Rasmi katika kongamano la Binti na Uongozi lililoandaliwa na Senati ya Vyuo na vyuo Vikuu UVCCM Mkoa wa Kusini Unguja Mbunge huyo wa vijana amemwakilisha mbunge wa viti maalum CCM mkoa wa kusini Unguja Mhe Wanu Hafidh Ameir ambaye pia ni  Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwanamke Initiatives Foundation inayofanya kazi kubwa ya kuwainua Mabinti na Vijana katika kukuza vipaji vyao vya uongozi, kiuchumi na kijamii. Washiriki kwa kauli moja wameazimia kushiriki kikamilifu kwenye Uchaguzi Mkuu katika kampeni, kupiga kura na kupigiwa kura kwa nafasi mbalimbali, pamoja na kuhakikisha wanafuata nyayo za Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan- Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na viongozi wengi wanawake katika uthubutu, uchapakazi, umahiri, utulivu, uvumilivu, tab...