Skip to main content

Posts

Showing posts from November 13, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mkurugenzi Kibaha Atoa Agizo Kurudiwa Kwa Uchongaji wa Barabara Mtaani Machinjioni na Kilimahewa

Na Mwandishi Wetu, Kibaha Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Rogers Shemwelekwa, ameonesha kutoridhishwa na utekelezaji wa mradi wa uchongaji wa barabara katika mitaa ya Machinjioni na Kilimahewa, na kuagiza kazi hiyo irudiwe mara moja ili iwe katika kiwango kinachokidhi malengo ya serikali. Dkt. Shemwelekwa ametoa agizo hilo tarehe 13/11/2025 katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika Kata ya Tangini, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi inayoendelea katika maeneo Kata mbalimbali ya Manispaa ya Kibaha. Amesema kuwa, barabara hizo ambazo zinagharimu shilingi milioni 30 kupitia mapato ya ndani ya Manispaa hiyo, hazijachongwa kwa ubora unaotakiwa na hivyo hazijakidhi lengo la serikali la kutatua kero za wananchi. “Ndugu viongozi, nimekagua mradi huu wa barabara na niseme wazi sijaridhishwa na kazi iliyofanyika. Lengo la serikali ni kutatua kero za wananchi, lakini kwa hali hii sioni kama tatizo limepatiwa suluhisho. Naagiza mtendaji wa kata kuhakikisha barabara hizi zin...

Mwigulu Nchemba: Kutoka kuchunga ng'ombe hadi Uwaziri Mkuu wa Tanzania

Mwigulu Lameck Nchemba Madelu ni Waziri Mkuu mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni mwenyeji wa mkoa wa Singida na kwa sasa ana umri wa miaka 50. Uteuzi wake umetangazwa rasmi bungeni mjini Dodoma, katikati mwa Tanzania  na baadaye kuthibitishwa na bunge, kwa mujibu wa Katiba ya nchi . Amethibitishwa kwa kura 369 za ndio kati ya 371 zilizopigwa na wabunge mbili zikiharibika. Mwigulu anajulikana kama mfano wa mafanikio yanayotokana na bidii na kujituma. Alikulia katika mazingira ya kijijini na alitoka katika familia yenye hali ya kawaida, ambapo aliwahi kuchunga ng'ombe nyikani akiwa kijana mdogo. Maisha hayo yalimfundisha nidhamu, uvumilivu na kuthamini kazi halali. Mara kadhaa amekuwa akisimulia hadithi ya maisha yake kama njia ya kuwahamasisha vijana kupambana kupitia elimu na kujituma. "Mimi umasikini wa Tanzania sijausoma kwenye kitabu nimeuishi, miaka takribani 32 nimeishi katika maisha hayo ya umasikini", alisema Nchemba mara baada ya kuthibitishwa bungeni. ...

Mwigulu Nchemba: Kutoka kuchunga ng'ombe hadi Uwaziri Mkuu wa Tanzania

Mwigulu Lameck Nchemba Madelu ni Waziri Mkuu mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni mwenyeji wa mkoa wa Singida na kwa sasa ana umri wa miaka 50. Uteuzi wake umetangazwa rasmi bungeni mjini Dodoma, katikati mwa Tanzania na baadaye kuthibitishwa na bunge, kwa mujibu wa Katiba ya nchi . Amethibitishwa kwa kura 369 za ndio kati ya 371 zilizopigwa na wabunge mbili zikiharibika. Mwigulu anajulikana kama mfano wa mafanikio yanayotokana na bidii na kujituma. Alikulia katika mazingira ya kijijini na alitoka katika familia yenye hali ya kawaida, ambapo aliwahi kuchunga ng'ombe nyikani akiwa kijana mdogo. Maisha hayo yalimfundisha nidhamu, uvumilivu na kuthamini kazi halali. Mara kadhaa amekuwa akisimulia hadithi ya maisha yake kama njia ya kuwahamasisha vijana kupambana kupitia elimu na kujituma. "Mimi umasikini wa Tanzania sijausoma kwenye kitabu nimeuishi, miaka takribani 32 nimeishi katika maisha hayo ya umasikini", alisema Nchemba mara baada ya kuthibitishwa bungeni. ...

ICGLR Yajipanga Kuimarisha Amani Katika Kanda

Imeelezwa kuwa Jumuiya ya nchi Wanachama wa Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) ni jukwaa sahihi la kupata ufumbuzi wa Kudumu wa changamoto zinazozikabili nchi wanachama kama vile ukosefu wa amani, usalama na maendeleo endelevu. Hayo yamebainishwa jijini Kinshasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Novemba 13, 2025 wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kawaida wa Mawaziri wa ICGLR uliofunguliwa na Waziri Mkuu wa DRC, Mhe. Judith Tuluka Suminwa.   Nchi wanachama zimetakiwa kuenzi Mkataba ulioanzisha Jumuiya hiyo unaolenga kufikiwa kwa amani, usalama na maendeleo ya kweli kupitia ushirikiano, umoja na mshikamano bila kusahau kujitoa na kujituma kwa hali na mali kupigania malengo hayo. Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo unaongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa.  Tanzania katika Mikutano huo inaunga mkono agenda zinazojadiliwa ikiwemo ya amani na usalama na kusisitiza kuwa itaendelea kutoa mchango mkubwa...

Dkt Mwigulu: Watumishi Wa Umma Kaeni Mguu Sawa

_▪️Awataka wawe tayari kuwezesha maendeleo, waende kwa gia ya kupandia mlima_ _▪️Amshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumteua_ WAZIRI MKUU, Mteule, Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka watumishi wa umma ambao ni wazembe, wala rushwa, wavivu na wazembe, wenye lugha mbaya kwa Wananchi wabadilike ili kuwezesha maono ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwaletea Watanzania maendeleo yaweze kutimia. “Watumishi wa umma na Watanzania wote tuwe tayari, lazima twende kwa gia ya kupandia mlima, lazima twende kwa gia ya kupita kwenye bahari yenye mawimbi, lazima twende kwa gia ya kupita kwenye anga lenye mawingu, lazima chombo kifike salama na watu wake wakiwa salama. Kwa watumishi wavivu, wazembe nitakuja na fyekeo na rato. Lazima maono ya Mheshimiwa Rais na ahadi ambazo amewaahidi Watanzania zitekelezwe.” Dkt. Mwigulu ameyasema hayo leo (Alhamisi, Novemba 13, 2015) bungeni jijini Dodoma alipokuwa akitoa  shukurani baada ya kuthibitishwa na Bunge kufuatia uteuzi wa Mhe...

Naibu Spika katika vazi rasmi

Naibu Spika wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Daniel Baran Sillo katika vazi rasmi la Naibu Spika wakati za zoezi la kupiga picha kwa mara ya kwanza mara baada ya kuchaguliwa. Mhe. Sillo amechaguliwa wakati wa Kikao cha Tatu cha Mkutano wa Kwanza wa Bunge la Kumi na Tatu uliofanyika leo Novemba 13, 2025 Jijini Dodoma.

Mhe Dkt Mwigulu apokelewa Ofisi ya Waziri Mkuu

Waziri Mkuu Mteule Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba alipopokelewa na watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, kwenye makazi ya Waziri Mkuu Mlimwa jijini Dodoma Novemba 13, 2025. Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba ameteuliwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania na kuthibitishwa na bunge.

Dk. Mwigulu Kuapishwa Kesho

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kesho tarehe 14 Novemba 2025 anatarajiwa kumuapisha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Taarifa ya Ikulu imesema kuwa hafla ya uapisho itafanyika Ikulu Chamwino jijini Dodoma kuanzia saa 10:00 asubuhi. Uteuzi wa Dkt. Mwigulu umefanyika baada ya jina lake kuthibitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Novemba 13, 2025. Kabla ya uteuzi huo, Dkt. Mwigulu alikuwa Waziri wa Fedha na Mipango. Anachukua nafasi ya Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ambaye amehitimisha kipindi cha miaka 10 cha utumishi wake kama Waziri Mkuu. Hafla hiyo inatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, wabunge, pamoja na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.