Mkazi wa Nkalalo wilayani Kiwmba mkoani Mwanza, Nicholaus James (21) amehukumiwa kifungo cha miaka 30 baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mwanafunzi wa kidato cha nne (jina linahifadhiwa) wa Sekondari ya Taro wilayani humo. Katika kesi hiyo ya Jinai namba 22882/2024, James ametiwa hatiani na Mahakama ya wilaya Kwimba kwa kosa la kumbaka binti ambaye utambulisho wake unahifadhiwa kwa sababu za kisheria (19) mwanafunzi wa kidato cha 4 shule ya sekondari Taro. Hukumu hiyo ilisomwa jana tarehe 16.12.2024 na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Kwimba, John Jagadi mbele ya mwendesha mashtaka wa Serikali Juma Kiparo. Awali, Mwendesha Mashtaka aliieleza Mahakama kwamba mshtakiwa alitenda kosa hilo tarehe 07.08.2024, katika Kijiji cha Nkalalo, wilaya ya Kwimba na mkoa wa Mwanza kinyume na vifungu vya 130(1)(2)(a) pamoja na kifungu cha 131(1) cha Kanuni ya Adhabu sura ya 16 ya sheria marejeo ya mwaka 2022. Mshtakiwa alifikishwa Mahakamani kwa mara ya kwanza tarehe 14.08.2024 ...
Marato tv - Sauti ya Jamii