Na Mwandishi Wetu, Muheza NAIBU Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo, Hamis Mwinjuma maarufu MwanaFA leo tarehe 19 2025, amekabidhi bati 120 kwa ajili ya kuezekea nyumba ya mtendaji wa Umoja wa vijana (UVCCM) wilayani Muheza. Akikabidhi bati hizo kwa Mwenyekiti wa UVCCM wilaya Muheza Aziza Mshakangoto, MwanaFA alisema ametekeleza ahadi yake ya kuziezeka nyumba tatu za jumuiya za chama wilayani hapa kuunga mkono wazo la Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Ustadh Rajab Abdarahman Abdallah za kila wilaya mkoani hapa kujenga nyumba za watumishi wa Chama. MwanaFA alisema kuwa katika kipindi cha miaka minne na nusu aliyokaa katika ubunge wilaya ya Muheza imepiga hatua ya maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo katika chama. Alisema mwaka 1993 waliokuwa viongozi wa CCM katika wilaya hiyo, walitenga eneo la Kirumba lililopo kata ya Genge kujengwa nyumba za watumishi wa chama pamoja na ofisi za chama. "Lakini Sasa ni miaka 32 watu walikuwa wanasema watajenga lakini hapakujengwa...
Marato tv - Sauti ya Jamii