▪️Awataka watumishi kutimiza wajibu wao_ Dodoma, Agosti 2, 2026 WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewahimiza watendaji wa Serikali kuwahudumia kikamilifu Watanzania ili miradi inayojengwa na Serikali itoe matokeo chanya. “Tunachokijenga hapa, si jengo pekee, bali tunajenga mazingira bora ya utendaji wa mfuko. Kupitia uwekezaji huu tunachochea na tunaharakisha utekelezaji wa dhamira ya dhati aliyoionesha Mheshimiwa Rais kumsaidia mkulima mdogo kwa kuwezesha kupata mikopo.” “Watumishi wote wanapaswa kutimiza wajibu wao kwa bidii ili uwekezaji huu uwe na manufaa kwa Taifa. Tusiweke ofisi nzuri halafu huduma zikawa duni, tutakua hatujafikia malengo yaliyokusudiwa, ofisi nzuri lakini mwananchi akija kupata huduma anaambiwa njoo kesho, njoo kesho, majengo haya hayatakuwa na maana,” amesema Waziri Mkuu. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili Agosti 2, 2026) Iyumbu jijini Dodoma wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa makao makuu ya ofisi za Mfuko wa Udhamini wa Pembejeo za Kilimo (A...
Marato tv - Sauti ya Jamii