Na OWM - TAMISEMI, Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amewataka walimu wapatao 150 wa shule za amali waliopatiwa mafunzo nchini India kwenda kuwapatia ujuzi vijana wa kitanzania katika shule wanazofundisha ambao utawawezesha kuwa wabunifu, wajasiriamali na washindani katika ajira za ndani na nje ya nchi ili kutoa mchango katika maendeleo ya taifa. Prof. Shemdoe ametoa wito huo Mei 04, 2026 wakati wa kikao chake na walimu hao wapatao 150 wa Shule za Amali ambao wamerejea nchini kutoka nchini India walihudhuria mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kutoa elimu ya ufundi na mafunzo ya stadi za kazi kama nyenzo muhimu ya kukuza uchumi wa viwanda, kupunguza ukosefu wa ajira kwa vijana, na kuongeza ushindani katika soko la ajira. “Tunategemea vijana watakaotoka katika shule za amali wawe na uwezo wa kushindana katika ajira za ndani na nje ya nchi, waweze kujiajiri na kuwa wajasiriamali wenye mc...
Marato tv - Sauti ya Jamii