Na Mwandishi Wetu WASANII ambao wameendelea kuchangamkia fursa ya kupima moyo bure katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), iliyotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan wamempongeza Rais kwa kuwapa fursa hiyo. Akizungumza wakati wa uchunguzi wa moyo kwa wasanii hao jana, Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Dk. Peter Kisenge alisema amefurahi kuona wasanii wanachangamkia fursa hiyo na kuwataka wengine kuendelea kujitokeza. “Nimemwona Zuchu, Mboso, D Voice wamekuja naomba nitumie fursa hii kuwashauri wasanii wengine waige mfano huu wa kuja kupima vipimo vya moyo bure,” alisema “Tunamshukuru sana Rais Samia kwa fursa hii ya kuwapima wasaniii bure hii ni kuhamasisha wananchi wote wawe na tabia ya kupima afya zao ili kuepuka magonjwa yasiyo ya kuambukiza ambayo yanachangia vifo vingi sana,” alisema Naye Mbwana Yusufu kutoka (WCB), maarufu kama Mboso alimshukuru Rais Samia kwa fursa hiyo akisema yeye anashida ya moyo na amekuwa akifanya vipimo mara kwa mara kujua maendeleo ya afya yake ya moyo. ...
Marato tv - Sauti ya Jamii