Na Mwandishi Wetu - Dodoma Wanafunzi waliokosa nafasi katika awamu ya kwanza ya udahili wa Shahada ya Kwanza sasa wamepata fursa nyingine baada ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kufungua Awamu ya Pili ya Udahili kwa mwaka wa masomo 2026/2027. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Septemba 8,2026 na Katibu Mtendaji wa TCU Prof. Charles Kihampa amesema awamu hiyo itafunguliwa hadi Septemba 21, 2026, huku waombaji ambao hawakuweza kukamilisha maombi au hawakupata nafasi katika awamu ya kwanza wakitakiwa kutumia fursa hiyo kuomba katika vyuo wanavyopenda. "Taarifa hiyo inakuja wakati ambapo idadi kubwa ya vijana imeonyesha uhitaji wa kuendelea na elimu ya juu nchini, katika awamu ya kwanza, jumla ya waombaji 149,645 waliomba kujiunga na vyuo 93 vinavyodahili wanafunzi katika Shahada ya Kwanza",amesema. Amesema idadi ya programu za masomo zilizowasilishwa pia imeongezeka kutoka 894 mwaka 2025/2026 hadi 1,019 mwaka huu ikiwa ni sawa na ongezeko la programu 125. "Wanafunzi z...
Marato tv - Sauti ya Jamii