Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Butiama Mhe. Jumanne Sagini amehudhuria Uzinduzi wa Kampeni za Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Butiama ambapo amemnadi na kumuombea kura za ndio Mgombea wa Urais kupitia tiketi ya CCM Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Mgombea ubunge wa Jimbo la Butiama Mhe. Dkt. Wilson Charles Mahera. Mhe. Sagini ameeleza kuwa kuna kila sababu ya mwananchi wa Butiama kumpa kura ya ndio Mgombea wa urais, ubunge na udiwani anayetokana na Chama Cha Mapinduzi ili kutengeneza muunganiko wa mafiga matatu ambayo yatarahisha kuleta maendeleo kama yalivyopatika katika kipindi chake cha 2020-2025. "Kipindi cha Mwaka 2020 Wilaya ya Butiama tuliongoza kutoa kura nyingi za Rais Mwaka 2025 tunaye Dkt. Samia Suluhu Hassan na Dkt. Wilson Mahera pamoja na madiwani wa Kata zote 18 wanaotokana na Chama Cha Mapinduzi msifanye kosa wapeni kura nyingi za ndio ili wanapoongea lugha moja maendeleo yanajaa ndani ya Butiama kwani Mhe. Rais Samia ni mtu wa huruma na nyie ni mashuhuda hatukua...
Marato tv - Sauti ya Jamii