Na. Edmund Salaho - Tanga Kamishna wa Uhifadhi TANAPA CPA Musa Nassoro Kuji ambaye pia ni mlezi wa HIFADHI SACCOS LTD ametoa wito kwa watumishi wote wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania kujiunga pamoja na kuanzisha SACCOS moja kwa watumishi wote wa TANAPA itakayoitwa TANAPA SACCOS LTD. Kamishna Kuji ameyasema hayo leo Septemba 24, 2025 katika Mkutano Mkuu wa mwaka 2025 wa HIFADHI SACCOS unaofanyika Jijini Tanga. "Ninafahamu kuwa kulikuwa na timu maalum ya uhamasishaji ambayo ilipita katika vituo vyote vya kazi kuhamasisha watumishi kufahamu faida za kuwa na SACCOS moja na kuwaomba watumishi wawe tayari kuunga mkono suala hilo muhimu. Mimi pia katika ziara zangu katika vituo vyote katika Shirika nimewasihi watumishi kukubali wazo la kuwa na SACCOS moja. Katika maeneo yote niliyopita, watumishi wamenihakikishia kuwa wazo hilo ni wazo jema na wapo tayari kuliunga mkono wakati ukifika". Akitaja faida chache zitakazopatikana kwa kuwa na SACCOS moja, Kamishna Kuji alibainisha k...
Marato tv - Sauti ya Jamii