Skip to main content

Posts

Showing posts from March 24, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MwanaFA awasilisha majibu ya haki za wasanii kwa Kamati ya bunge

Na Mashaka Mhando, Dodoma NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (MwanaFA), leo ameongoza ujumbe wa Wizara mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuwasilisha na kujadili majibu ya hoja za Bunge kuhusu Sheria ya Haki ya Kunufaika na Mauzo Endelevu (Resale Right) ya mwaka 2025. Uwasilishaji huo wa leo, Machi 25, 2026, unalenga kutoa ufafanuzi wa kina juu ya kanuni na taratibu zitakazomwezesha msanii wa Tanzania kuendelea kupata mirabaha (Royalty) kila mara kazi yake inapouzwa tena sokoni na mtu mwingine baada ya mauzo ya awali. Akizungumza mbele ya Kamati hiyo jijini Dodoma, Mhe. Mwinjuma amebainisha kuwa Wizara imefanyia kazi hoja zote zilizoibuliwa na Bunge ili kuhakikisha sheria hiyo ndogo inakuwa na tija na inatekelezeka bila vikwazo kwa wadau wa kazi za sanaa na ubunifu. Mhe. Naibu Waziri ameeleza kuwa Wizara imefanya uchambuzi wa kina wa hoja za Bunge ili kuhakikisha sheria hiyo ndogo inakidhi vigezo vya kisheria na inatekelezeka bila k...

Tanzania Development Bank welcomes the new EADB new Country Manager in Dar to strengthening cooperation

By Prosper Makene  The Tanzania Development Bank (TIB) has welcomed the new Country Manager of the East African Development Bank (EADB), Ms. Angela Muga, on an official visit aimed at strengthening cooperation between development finance institutions in the East African region. The visit underscored the commitment of both institutions to fostering sustainable economic growth, sharing experiences, and promoting regional integration. During her visit, Ms. Muga was accompanied by a delegation from EADB, led by Mr. Stephen Wambura, the EADB Resident Manager for Tanzania.  The delegation took the opportunity to visit Pipes Industries, a key beneficiary of joint financing from TIB and EADB. Located in the Vingunguti Industrial Area in Dar es Salaam, Pipes Industries is a leading manufacturer of plastic pipes and other plastic products essential for infrastructure development. Pipes Industries received a loan of approximately TSh 28.65 billion, which has significantly contributed to ...

Benki ya TIB Yapokea Ugeni kutoka EADB, Wafanya Ziara Pipes Industries

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Benki ya Maendeleo (TIB) leo ilimkaribisha rasmi Meneja Mkazi (Country Manager – Kenya) mpya wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), Bi. Angela Muga na ujumbe wake kwa ziara maalumu yenye lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Taasisi za Fedha za Maendeleo (DFIs) katika ukanda wa Afrika Mashariki. Katika ziara hiyo iliyoambatana na ujumbe kutoka benki ya EADB, imeonyesha dhamira ya pamoja ya kuharakisha ukuaji endelevu wa uchumi, kubadilishana uzoefu, ujenzi wa viwanda na ujumuishaji wa kikanda katika eneo la Afrika Mashariki. Ujumbe wa Bi. Muga ukiongozwa na mwenyeji wake Bw. Stephen Wambura ambaye ni Meneja Mkazi EADB Tanzania, pia ulipata nafasi ya kufanya ziara katika kiwanda cha kuzalisha mabomba ya plastiki cha Pipes Industries kilichopo eneo la viwanda la Vingunguti jijini Dar es Salaam ambapo kiwanda hicho ni mnufaika muhimu wa ufadhili huo wa pamoja. Kiwanda cha Pipes Industries kilipokea mkopo wa takribani Shilingi za kitanzania Bil...

Katibu UVCCM Pangani aanza ziara ya "Operesheni Samia"

Na: Mwandishi Wetu, Pangani Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Pangani mkoani Tanga, Nasri Mkalipa, ameanza ziara ya kuimarisha uhai wa Chama na kusikiliza kero za wananchi, ziara iliyopewa jina la "Operesheni Samia." Mkalipa ameanza ziara hiyo Machi 24, 2026, katika Kata za Mkalamo na Mkwaja ambapo ameonana na makundi mbalimbali ya kijamii ikiwa ni utaratibu wa CCM wa kuwafikia wananchi kule walipo, kusikiliza na kutatua kero zao kwa wakati. Akiwa ziarani humo, Mkalipa amewaasa vijana kujiunga katika vikundi ili kunufaika na mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri. "Vijana wenzangu tujiunge katika vikundi ili tuweze kunufaika na mikopo. Rais wetu na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dk. Samia Suluhu Hassan anatoa fedha nyingi za mikopo, ni jukumu letu vijana kuchangamkia fursa hizo," amesema Mkalipa.  Sambamba na hilo, Mkalipa amewaeleza vijana kujiandaa kwa ujio wa mashindano ya mpira wa miguu yaliyopewa jina la Aweso Vijana Cup. ...

Katambi Awasilisha Utekelezaji na Bajeti 2024/2025/ 2026

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mheshimiwa Patrobas Katambi (MB), amewasilisha Taarifa  ya Utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026 pamoja na kuwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Amewasilisha Taarifa ya Wizara,Jeshi la Polisi, Magereza, Uhamiaji,Zimamoto na Uokoaji na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA), mbele ya  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama(NUU). Taarifa hizo zimewasilishwa katika Ukumbi wa Herman Stewart,Bungeni jijini Dodoma.

Katibu Mkuu CCM Ziarani Uchina

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Asha-Rose Migiro, anaondoka nchini leo kuelekea Beijing, Jamhuri ya Watu wa China, kwa ziara ya kikazi ya siku sita kufuatia mwaliko wa Chama cha Kikomunisti cha China. Ziara hiyo inalenga kuendeleza na kuimarisha uhusiano wa kihistoria na ushirikiano wa karibu uliopo kati ya Chama Cha Mapinduzi na Chama cha Kikomunisti cha China.  Ziara hii inafanyika katika kipindi ambacho mwaka 2026 umetangazwa rasmi kuwa mwaka wa kukuza uhusiano na maelewano ya kijamii na kitamaduni kati ya China na Afrika. Hivyo, mwaka huu unatoa fursa adhimu ya kuimarisha urafiki, kubadilishana uzoefu na kujenga uelewano wa pamoja kati ya vyama hivi viwili. Katika ziara hiyo, Katibu Mkuu ataambatana na ujumbe wa watu watano.  Akiwa nchini humo, yeye pamoja na ujumbe wake watafanya mazungumzo na viongozi wa juu wa Chama cha Kikomunisti cha China.

Serikali imenunua Ndege Kwa Ajili ya Kulinda Mazao ya Wakulima Nchini

 Na, Saleh Lujuo-Dodoma KATIKA Jitihada za Kudhibiti ndege waharibifu wa Mazao ya Wakulima pamoja na visumbufu vya mazao, Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) imenunua ndege nyuki za kisasa kwa ajili ya kuboresha ufuatiliaji na udhibiti wa visumbufu vya mazao mashambani ikiwa ni hatua ya kudhibiti visumbufu hivyo kabla havijasababisha madhara kwa wakulima.  Hatua hiyo inalengo kumfanya Mkulima Kuvuna mazao yake kwa Tija na kuyafanya mazao hayo kuwa Bora ili kupata soko lenye uhakika ndani na nje ya nchi. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Prof. Joseph Ndunguru ameyasema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu masuala yanayohusiana na taasisi hiyo leo Machi 24, 2026, katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) uliopo katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.  Amesema Mamlaka hiyo kwa sasa wana jumla ya ndege nyuki 21 na wako katika hatua za kukamilisha ununuzi wa ndege nyuki zingine 20. "hatua hii...

Mgodi wa Kihistoria Wa Niobium Kujengwa Mkoani Mbeya

▪️Ni Mradi wa Panda Hill wa Niobium utakaogharimu TSh 700 bn ▪️Ni uwekezaji unaohusisha Kampuni ya Denham ya Marekani. ▪️Rais Samia apongezwa kufanikisha mradi wa uchimbaji Niobium ▪️Kiwanda cha kuyeyusha ferroniobium kitakachojengwa Tanzania kitakuwa cha nne duniani ▪️Waziri Mavunde asema Tanzania kuchangia takriban asilimia 4 ya uzalishaji wa Niobium na uzalishaji wa takriban tani 100,000 kwa mwaka ▪️Ajira  kufikia takriban  watu 7,000 MBEYA, Machi 24, 2026. Tanzania imeingia hatua muhimu ya kuimarisha biashara na Marekani baada ya Serikali na Panda Hill Tanzania Limited kusaini mkataba wa makubaliano ya kuendeleza Mradi wa Niobium wa Panda Hill, hatua inayolenga kuifanya Mbeya kuwa kitovu cha uzalishaji na usindikaji wa madini mkakati. Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde alisema mradi huo ni wa uzalishaji wa madini adimu ambayo hayapatikani kila mahali duniani, na kwamba Tanzania inalenga kuchukua nafasi ya kipekee katika soko la kimat...