Skip to main content

Posts

Showing posts from May 19, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Njombe Yaibuka Kitovu Cha Madini Adimu, Soko Lake Kuu Lipo China

📍Njombe Serikali imetangaza kuwa Mkoa wa Njombe unatarajiwa kuwa kitovu kipya cha uwekezaji wa madini nchini baada ya kugunduliwa kwa madini adimu ya Rare Earth Elements (REE) ya aina mbili ambayo ni Neodymium Nd na Praseodymium Pr yenye mahitaji makubwa katika teknolojia za kisasa duniani. Akizungumza katika kijiji cha Mkiu Wilaya ya Ludewa, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Njombe, Mhandisi Lucas Mlekwa, amesema utafiti wa madini hayo unaendelea kufanywa na kampuni ya Hongji Mining Co. Ltd kwa kushirikiana na wazawa, huku soko kubwa la madini hayo likiwa nchini China kutokana na ukuaji wa haraka wa sekta ya viwanda na teknolojia. Amesema madini ya REE yanatumika katika utengenezaji wa betri za magari ya umeme, mitambo ya kuzalisha umeme wa upepo pamoja na vifaa mbalimbali vya kielektroniki vinavyotumika duniani kote. “Mkoa wa Njombe unaendelea kufungua ukurasa mpya wa maendeleo kupitia rasilimali hizi muhimu ambazo zina mchango mkubwa katika mapinduzi ya teknolojia ya kijani duniani,” a...

Duce Yageuka Kitovu Cha Ubunifu na Teknolojia

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Dkt. Aneth Komba, amezitaka taasisi za elimu ya juu nchini kuhakikisha tafiti, ubunifu pamoja na matumizi ya teknolojia vinaelekezwa katika kutoa suluhisho la changamoto halisi zinazowakabili wananchi na kuchochea maendeleo ya taifa. Dk. Komba alisema hayo wakati akifungua Maadhimisho ya Wiki ya 11 ya Utafiti na Ubunifu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kishiriki cha Elimu (DUCE), yaliyowakutanisha wanafunzi, wahadhiri, watafiti, wabunifu pamoja na wadau mbalimbali wa elimu na maendeleo. Aidha, alieleza utayari wake wa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kishiriki cha Elimu (DUCE), Taasisi ya Global Education Link (GEL) pamoja na wadau wengine wa elimu nchini katika kuimarisha mwongozo wa taaluma kwa wanafunzi na walimu ili kuwaandaa vijana kuendana na mahitaji ya dunia ya sasa na ya baadaye. Utayari huo umeelezwa na Dkt. Komba wakati alipotembelea banda la Global Education Link katika maadhimisho hayo, am...

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 Aipongeza REA Uhamasishaji wa Nishati Safi ya Kupikia

📍*Madaba, Ruvuma* Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2026 ,Ndugu Wazo Michael Mwang’onda ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa juhudi kubwa inazoendelea kuzifanya katika utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia nchini, akieleza kuwa miradi hiyo imekuwa na mchango mkubwa katika kuhamasisha wananchi kutumia nishati safi, salama na rafiki kwa mazingira. Pongezi hizo amezitoa wakati alipotembelea banda la REA katika maonesho yanayoendelea sambamba na Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma, ambapo alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na wakala huo katika kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanapata huduma ya nishati safi ya kupikia kwa gharama nafuu. Akizungumza mara baada ya kutembelea banda hilo, kiongozi huyo amesema REA imeendelea kuwa chachu muhimu katika utekelezaji wa ajenda ya taifa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi pamoja na kuweka mazingira wez...

Tanzania Takes Center Stage at WHA79 as UHC Tops Agenda*

By John Mapepele _Geneva, Switzerland_   The Minister of Health of Tanzania, Hon. Mohamed Mchengerwa, has led the Government of Tanzania delegation at the official opening of the 79th World Health Assembly (WHA79), which began today, May 18, 2026, in Geneva, Switzerland. This major global health conference, bringing together more than 180 countries from different parts of the world, was officially opened by Tedros Adhanom Ghebreyesus, Director-General of the World Health Organization (WHO). “The 79th World Health Assembly is being held from May 18 to 23, 2026, in Geneva, Switzerland. The meeting brings together delegates from WHO Member States to address major pressures facing health systems and to establish global health policies, with strong emphasis on universal health coverage, mental health, and the impact of climate change on health,” explained Hon. Mchengerwa. According to Hon. Mchengerwa, the main discussion areas during the 2026 meeting include Universal Health Covera...

Zungu atoa saluti kwa vyombo vya ulinzi nchini, aipongeza bajeti ya trilioni 4.28 kwa Wizara ya Ulinzi na Jkt

Bunge limepitisha bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) yenye thamani ya Shilingi Trilioni 4.28 kwa mwaka wa fedha 2026/2027, huku Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu, akiipongeza Serikali kwa kuendelea kuimarisha sekta ya ulinzi na usalama nchini. Akizungumza Mei 19, 2026 bungeni Jijini Dodoma mara baada ya kupitishwa kwa bajeti hiyo, Zungu alisema ameridhishwa na kazi kubwa inayofanywa na Wizara ya Ulinzi pamoja na vyombo vya ulinzi katika kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa kisiwa cha amani, utulivu na usalama. Spika huyo alimpongeza Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Rhimo Nyansaho, kwa uongozi wake madhubuti na usimamizi mzuri wa wizara hiyo nyeti, akieleza kuwa utekelezaji wa majukumu ya wizara umeendelea kuleta mafanikio makubwa kwa taifa. “Tunajivunia kazi kubwa inayofanywa na vyombo vyetu vya ulinzi katika kulinda mipaka ya nchi, kudumisha amani na kuhakikisha wananchi wanaendelea kuwa salama muda wote,” alisema Zungu. Aidha, amewapongeza pia viong...

Dkt. Mwigulu Ataka Asilimia 20 ya Mapato ya Mazao Ielekezwe Kujenga Maghala

_▪️Azindua Mkakati wa Uhamasishaji wa Matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala_ _▪️Ataka wakulima walipwe fedha za awali badala ya kukopwa mazao_ _▪️Aagiza matumizi ya lumbesa yakomeshwe katika biashara ya mazao_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema asilimia 20 ya mapato yatokanayo na mazao ya kilimo inapaswa kuelekezwa katika ujenzi wa maghala karibu na maeneo ya uzalishaji ili kupunguza gharama kwa wakulima na kuongeza ufanisi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala nchini. “Asilimia 20 ya mapato yanayotokana na mazao ya kilimo inapaswa kuelekezwa katika ujenzi wa maghala kwenye maeneo ya uzalishaji ili wakulima wasipate shida ya kusafirisha mazao yao umbali mrefu,” amesema. Waziri Mkuu amesema hayo leo Mei 19, 2026 alipokuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma, yenye kaulimbiu isemayo “Mfumo Imara, Uchumi Endelevu.” Katika hafla hiyo, Waziri...

Balozi Matinyi Awasili Algeria

Balozi Mobhare Matinyi amewasili jijini Algiers, Jumanne, tarehe 19 Mei, 2026, tayari kuanza majukumu ya kuiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria. Balozi Matinyi alilakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Houri Boumediene na Mwenyekiti wa Mabalozi wa nchi wanachama za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) waliopo Algeria, Balozi Ndumiso Ndima Ntshinga wa Afrika Kusini; Balozi Toko Diakenga Serão wa Angola; na Balozi Abdellatif Al-Layeh wa Misri pamoja na watumishi wa Ubalozi wa Tanzania wakiongozwa na Kaimu Balozi Suleiman Mussa Rashid. Balozi Matinyi aliteuliwa na kutangazwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mnamo tarehe 24 Aprili, 2026, kuwa Balozi wa Tanzania nchini Algeria baada ya kuitumikia nafasi hiyo jijini Stockholm katika Ufalme wa Sweden tangu Mei 2025. Mbali ya Algeria, Ubalozi wa Tanzania jijini Algiers huiwakilisha Tanzania pia katika nchi za Tunisia, Niger, Mauritania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Ki...

Dkt. Mwigulu Ataka Asilimia 20 ya Mapato ya Mazao Ielekezwe Kujenga Maghala

_▪️Azindua Mkakati wa Uhamasishaji wa Matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala_ _▪️Ataka wakulima walipwe fedha za awali badala ya kukopwa mazao_ _▪️Aagiza matumizi ya lumbesa yakomeshwe katika biashara ya mazao_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema asilimia 20 ya mapato yatokanayo na mazao ya kilimo inapaswa kuelekezwa katika ujenzi wa maghala karibu na maeneo ya uzalishaji ili kupunguza gharama kwa wakulima na kuongeza ufanisi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala nchini. “Asilimia 20 ya mapato yanayotokana na mazao ya kilimo inapaswa kuelekezwa katika ujenzi wa maghala kwenye maeneo ya uzalishaji ili wakulima wasipate shida ya kusafirisha mazao yao umbali mrefu,” amesema. Waziri Mkuu amesema hayo leo Mei 19, 2026 alipokuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma, yenye kaulimbiu isemayo “Mfumo Imara, Uchumi Endelevu.” Katika hafla hiyo, Waziri...