□ Timu yasheheni wataalamu wa kifedha, madini, wanasheria na wachimbaji. ▪️Lengo ni kuhakikisha watanzania wanajengewa uwezo wa kimtaji kwenye sekta ya madini □ Asema ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Dkt. Samia S. Samia kutengeneza mabilionea watanzania 📍 Dodoma Katika hatua ya kuimarisha sekta ya madini na kuwawezesha wachimbaji wadogo nchini kunufaika zaidi na rasilimali za madini, Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ameteua timu maalum ya wataalam kutoka Serikalini na sekta binafsi kwa ajili ya kuishauri Wizara ya Madini namna bora ya kuwainua wachimbaji hao kiuchumi kupitia uchimbaji wenye tija. Akizungumza jijini Dodoma leo Aprili 9, 2025, Waziri Mavunde amesema timu hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyetoa wito kwa Wizara kuhakikisha sekta ya madini inapiga hatua huku wachimbaji wadogo wakichimba kwa tija na manufaa makubwa zaidi na hivyo kuwajenga kiuchumi zaidi. “Kutokana na umuhimu wa...