Skip to main content

Posts

Showing posts from October 12, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Oktoba 29 inakaribia, ewe mwananchi usipange kukosa kupiga kura

Na: Dkt. Reubeni Lumbagala, Tanga Kila baada ya miaka mitano nchi yetu inafanya Uchaguzi Mkuu wa kuchagua viongozi katika nafasi za Urais, Ubunge na Udiwani ili kuwatumikia wananchi. Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imeshatangaza Jumatano ya Oktoba 29, 2025 kuwa ndiyo siku ya Uchaguzi Mkuu. Katika siku hii, wananchi wanapata fursa ya kwenda kupiga kura katika vituo walivyojiandikisha ili kutimiza haki yao ya kikatiba ya kuchagua viongozi ambao ni muhimu katika kufanikisha mipango ya maendeleo. Vituo vya kupigia kura vitafunguliwa kuanzia saa moja kamili asubuhi na kufungwa saa kumi kamili jioni. Katika masaa haya kumi, wananchi waliojiandikisha wanapata fursa ya kipekee ya kuamua hatma ya maisha yao katika kipindi cha miaka mitano ijayo yaani 2025-2030. Kwa kuzingatia ukweli kuwa siasa inaamua hali ya maisha ya wananchi itakavyokuwa, ni muhimu sana kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura kuchagua viongozi ambao wanadhani wanafaa katika kuwatumikia. Katika Uchaguzi Mkuu huu, ...

Tarura yatekeleza Miradi Mikubwa ya Miundombinu ya Barabara ya Bilioni 302.95

#Katika kipindi cha Miaka Minne  Dodoma Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Mhandisi Victor Seff amesema katika kipindi cha miaka minne (4) ya Serikali ya Awamu ya Sita, Wakala umekamilisha ujenzi wa miradi mikubwa ya miundombinu ya barabara za Wilaya yenye thamani ya Shilingi Bilioni 262.46 huku miradi yenye thamani ya Shillingi Bilioni 40.49 ikiwa katika hatua mbalimbali za utekelezaji na miradi yote ikikamilika itakuwa na thamani ya Shilingi Bilioni 302.95. Mhandisi Seff amesema mafanikio hayo yametokana na ongezeko la bajeti lililofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita kwa TARURA ambapo awali walikuwa wakipokea bajeti ya Shilingi Bilioni 275 kwa mwaka lakini baada ya Serikali ya Awamu ya Sita kuona kazi kubwa ya TARURA bajeti iliongezeka kutoka Bilioni 275 kwa mwaka hadi kufikia Shilingi Trilioni 1.1 sawa na ongezeko la asilimia 230. “Baadhi ya miradi iliyokamilika ni ujenzi wa barabara za lami Kilomita 58.5 katika mji wa Serikali Mtumba-Dodoma, dar...

Madaktari bingwa wa Tanzania wahudumia waComoro 3,653

………. 20 wafanyiwa upasuaji mkubwa na wengine wapata rufaa kuja Dar Na Mwandishi Wetu, Anjouan  Comoro BALOZI wa Tanzania nchini Comoro, Saidi Yakubu, amewahakikishia wananchi wa Visiwa vya Comoro kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana nao katika sekta ya afya, hususan katika utoaji wa huduma za kibingwa, mafunzo kwa wataalamu wa afya, na uratibu wa rufaa za wagonjwa wanaohitaji matibabu maalum nchini Tanzania. Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga Kambi Maalum ya Matibabu ya Kibingwa iliyofanyika katika Hospitali ya Bambao, Anjouan, Balozi Yakubu alisema Serikali ya Tanzania itaendeleza jitihada za kuimarisha urafiki na ushirikiano wa afya kati ya mataifa hayo mawili kwa lengo la kuinua ubora wa huduma za afya kwa wananchi wa Comoro. “Urafiki wetu na Comoro umejengwa katika misingi ya utu, taaluma na dhamira ya pamoja ya kuhudumia binadamu,” alisema Balozi Yakubu. “Tanzania itaendelea kushirikiana na Comoro katika kujenga mifumo imara ya afya kwa manufaa ya wananchi wetu wote.” ali...

Ujenzi Skimu 738 za umwagiliaji, Dkt. Samia utaacha alama isiyofutika sekta kilimo

  Na: Dkt. Reubeni Lumbagala Kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania. Hii inatokana na ukweli kuwa kilimo kimeajiri Watanzania wengi zaidi ya asilimia 60 hasa waishio maeneo ya vijijini. Kutokana na kilimo kuwa na tija, wananchi waishio maeneo ya mjini nao siku hizi wanajishughulisha na kilimo kidogo (small scale agriculture) katika makazi yao hasa kilimo cha mbogamboga na matunda. Kimsingi, kilimo kina tija ukizingatia kinaacha athari chanya ya moja mwa moja hasa katika kuwapatia wananchi chakula na fedha. Kwa nchi yetu ya Tanzania ambayo tunakubaliana kuwa kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wetu, kama nchi hatuna budi kuweka mikakati madhubuti inayotekelezeka ili kuhakikisha tunakuza kilimo chetu ili kugusa kundi kubwa la wananchi ambao wamejiajiri katika sekta hii. Ikumbukwe kuwa sekta ya kilimo imefungamanishwa pia na sekta za ufugaji na uvuvi. Umuhimu wa sekta ya kilimo hauishii tu kutupatia chakula na fedha lakini pia kilimo kina mnyororo mkubwa wa thamani. Kupitia...

Balozi Matinyi aongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Biashara kati ya Nchi za Nordic na Afrika Jijini Oslo

Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Balozi Mobhare Matinyi, tarehe 9 Oktoba 2025, aliongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Biashara kati ya nchi za Nordic na Afrika uliofanyika jijini Oslo, Norway. Akifungua mkutano huo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway, Andreas Motzfeldt Kravik, alieleza kuwa ni muhimu nchi za Nordic na Afrika ziwe na sera rafiki za pamoja za kuboresha mazingira ya biashara na kuimarisha ushirikiano kati ya sekta za umma na binafsi katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati, na kwamba bara la Afrika linabeba mustakabali wa dunia. Washiriki wa mkutano huo unaofanyika kila mwaka walitoka sekta binafsi, jumuiya za wafanyabiashara, viongozi wa serikali, wanadiplomasia na washiriki wengine kutoka asasi za nchi mbalimbali duniani ikiwemo Marekani. Kaulimbiu ya mkutano huo ilijikita katika kuhamasisha biashara, matumizi ya nishati safi, na ushirikiano wa kuimarisha miundombinu kati ya nchi za Nordic na Afrika. Ujumbe wa Tanzania chini ya Balozi Matinyi ulimjumu...

Ziara ya Dkt Samia Mikoa ya Kanda ya Ziwa Imepata Mafanikio Makubwa-Msama

Mkurugenzi wa Msama Promotions na kada mtiifu wa CCM, Alex Msama Mwita amepongeza na kutoa maoni thabiti kufuatia ziara ya Mgombea Urais kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, mkoani Mara na Kanda ya Ziwa kwa ujumla. Alex Msama amesema; "Kwanza nimpe pole sana Dkt. Samia kwa uchovu wa mizunguko ya nchi nzima, akinadi sera za Ilani ya uchaguzi ya CCM kwa wananchi, lakini pia nimpongeze mno, amekuwa mahiri katika kutoa hoja nzito za namna gani CCM imejipanga kuwahudumia Watanzania. "Wananchi wa Kanda ya Ziwa, wakiwemo wa Mkoa wa Mara ninakotoka mimi, waliaminishwa upuuzi wa eti Rais Samia hapendwi, ujinga huo wameukataa kwa kujitokeza kwa wingi mno katika mikutano ya Dkt. Samia, Mikoa yote ya Mwanza, Simiyu na Mara," alisema Alex Msama na kuongeza; "Nichukue nafasi hii kumpongeza sana Dkt. Samia kwa sera nzuri alizozinadi Kanda ya Ziwa, hususan Mkoa wa Mara, mimi Alex Msama nilikuwepo Musoma, hakika nilifurahishwa mno na wingi wa Wananchi waliojitokeza kusikiliza sera...

Rais Dkt Samia yupo tayari kufanya mambo makubwa kwa wenye uliemavu - Majaliwa

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan yupo tayari kuendelea kufanya mambo makubwa kwa watu wenye ulemavu ili kukuza ustawi wa jamii hiyo kwa kuwawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo. Amesema hayo Oktoba 11, 2025 wakati wa hafla ya kupokea tuzo kwa niaba ya Rais Dkt. Samia ya  ya kutambua mchango wake katika kusimamia ustawi wa jamii ya watu wenye ulemavu nchini, kwenye hafla iliyofanyika kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay Jijini Dar es Salaam. Tuzo imetolewa na taasisi ya Foundation for Disabilities Hope (FDH)   Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia ameahidi kuendelea kuwahudumia watu wenye ulemavu kwa kuwa ana nia ya dhati ya kuona jamii hiyo inakuwa na ustawi utakaowawezesha kutumia fursa zilizopo kujikwamua kiuchumi. “Rais wetu anataka kuona watu wenye ulemavu wanafanya mambo kwa uhuru mkubwa”  “Ndugu washiriki, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya mengi sana,nataka niwaambie amenihak...

Rais Dkt. Samia Yupo Tayari Kufanya mambo Makubwa kwa wenye Ulemavu-Majaliwa

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan yupo tayari kuendelea kufanya mambo makubwa kwa watu wenye ulemavu ili kukuza ustawi wa jamii hiyo kwa kuwawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo. Amesema hayo Oktoba 11, 2025 wakati wa hafla ya kupokea tuzo kwa niaba ya Rais Dkt. Samia ya  ya kutambua mchango wake katika kusimamia ustawi wa jamii ya watu wenye ulemavu nchini, kwenye hafla iliyofanyika kwenye makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay Jijini Dar es Salaam. Tuzo imetolewa na taasisi ya Foundation for Disabilities Hope (FDH) Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia ameahidi kuendelea kuwahudumia watu wenye ulemavu kwa kuwa ana nia ya dhati ya kuona jamii hiyo inakuwa na ustawi utakaowawezesha kutumia fursa zilizopo kujikwamua kiuchumi. “Rais wetu anataka kuona watu wenye ulemavu wanafanya mambo kwa uhuru mkubwa” “Ndugu washiriki, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya mengi sana,nataka niwaambie amenihakikishia kuwa ...