Skip to main content

Posts

Showing posts from January 2, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dkt. Mwigulu Akagua Athari za Mvua, Kidete

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amekagua hali ya athari iliyosababishwa na mvua katika eneo la kidete, Kilosa mkoani Morogoro. Akiwa eneo hilo Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amewahakikishia wakazi wa eneo hilo kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ilishachukua hatua za kukabiliana na mvua kwa kuamua kujenga mabwawa katika eneo hilo.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Akutana na Kufanya Mazungumzo na Balozi wa India Nchini Tanzania

Waziri wa ulinzi na JKT mheshimiwa Dkt Rhimo Nyansaho (Mb) , tarehe 02 Januari 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na balozi wa India nchini Tanzania , Mheshimiwa Bishwadip Dey katika ofisi ndogo za wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Upanga jijini Dar-es-salaam.

Hakikisheni Mradi wa Bwawa la Maji Kidunda Hausimami - Dkt Mwigulu

WAZIRI MKUU Dkt Mwigulu Nchemba ameiagiza Wizara ya Maji kuhakikisha mradi wa Bwawa la Maji Kidunda hausimami na unakamilika kwa wakati ili uanze kutoa huduma ya maji kwa wananchi. Ametoa wito huo leo (Ijumaa, Januari 02, 2026) wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa bwawa hilo lililopo Wilaya ya Morogoro, mkoani Morogoro.  Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Dkt. Mwigulu amesema kuwa mradi huo unaakisi maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha anakabiliana na changamoto ya upungufu wa maji hasa kutokana na mabadiliko ya tabianchi. “Kiongozi wetu anaona mbali; aliamua kuutekeleza mradi huu katika kipindi ambacho kulikuwa na utekelezaji wa miradi mingine mikubwa na ya kimkakati iliyotumia fedha nyingi. Serikali inachukua hatua ili kukabiliana na changamoto za Watanzania.” Wakati huohuo, Dkt. Mwingulu ameiagiza Wizara ya Maji wahakikishe wanaandaa jedwali litakalomsaidia mkandarasi katika utekelezaji wa mradi huo ili uweze kukamilika kwa wakati. Kwa upande wake, Waziri wa Ma...

Dkt. Mwigulu Azungumza na Wananchi Walioathiriwa na Mvua Kilosa

_Autaja mradi wa ujenzi wa mabwawa ya kuhifadhi maji ya Mvua eneo la Kidete._ Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amezungumza na wakazi wa Tindiga wilaya ya kilosa mkoani Morogoro ambao wameathirika na mvua zinazoendelea kunyesha nchini. Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amewaeleza wakazi hao kuwa Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ilishaanza mikakati ya kukabiliana na athari za mvua katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa morogoro kwa kutekeleza mradi wa ujenzi wa Mabwawa eneo la Kidete. Amesema kuwa ujenzi wa mabwawa hayo ya maji yatakuwa ni suluhisho la kudumu ya mafuriko katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Morogoro. Ameongeza kuwa kwa sasa mpango huo upo katika hatua za kitalaam ikiwemo kumpata mkandarasi. ”Fedha imepatikana kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa kwa sasa tunaendelea na taratibu za kitaalam, Wizara zinazohusika hakikisheni mnakamilisha taratibu hizo ili ujenzi uanze”

Dkt. Mwigulu Akagua Maendeleo Mradi wa Bwawa la Maji Kidunda

Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba leo Januari 02, 2026 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Bwawa la Maji Kidunda lililopo Mkoani Morogoro. Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Dkt. Mwigulu amesema kuwa mradi huo unaakisi maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha nchi inakabiliana na changamoto ya upungufu wa maji hasa kutokana na mabadiliko ya tabia nchi. Pia, ameiagiza Wizara ya Maji kuhakikisha mradi huo hausimami na unakamilika kwa wakati ili uanze kutoa huduma ya maji kwa wananchi.

Mwenyekiti wa Uvccm Mkoa wa Kagera Amwaga Pongezi Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Kagera Faris Buruhan amempongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo ameendelea kuliongoza Taifa kwa uvumilivu na ustahimilivu, hata pale zinapotokea changamoto mbalimbali ameweza kuzitafutia ufumbuzi kwa hekima na busara. Alisema hayo wakati wa Dua maalum aliyoiandaa mwenyekiti huyo kwa ajili ya kuliombea Taifa,Rais Dk.Samia na wasaidizi wake amayo imefanyika katika kata ya Katoro Bukoba vijijini na kuhudhuliwa na viongozi wa dini,Serikali,baadhi ya wabunge na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa na nje. "Dk.Samia ameonyesha uongozi na ukomavu kwa kipindi cha miaka minne iliyopita na sasa baada ya uchaguzi wananchi ni mashahidi tumpe moyo,nguvu na kuendelea kusimama kumsemea pale wanapotokea wapotoshaji maana ushahidi upo hususani miradi mikubwa ya maendeleo iliyotekelezwa katika maeneo yetu"Faris Alitoa mfano kwa shule aliyosomea ya Katoro sekondari kipindi ...