WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote yaliyofanywa na mbunge wa Peramiho mkoani Ruvuma, Marehemu Jenista Mhagama kuweka ushiriki kati ya Serikali na taasisi ya kidini. Amesema marehemu Jenista alikuwa mpatanishi akiunganisha fedha mbalimbali za pamoja na Serikali ambapo hadi leo wanaushirikiano mkubwa, pia aliimarisha umoja na mshikamano kati ya Serikali na sekta binafsi na kazi hiyo kwa uadilifu mkubwa. “Marehemu Jenista amekuwa anaamini katika mafanikio na hiyo ndio iliyompa jina la kiraka kwa kuwa kila nafasi aliyopewa aliimudu kwa ukamilifu. Jenista amegusa maisha ya wengi, mimi nilikuwa nashirikiana naye katika masuala ya uongozi na alikuwa mmoja wa marafiki wa familia.” Ameitoa kauli hiyo leo Jumatatu, Desemba 15, 2025, wakati akiwasilisha salamu za Serikali aliposhiriki Ibada ya kuaga mwili wa Marehemu Jenista Mhagama iliyofanyika katika kanisa Katoliki la Abasia ya Mtakatifu Benedicto, Peramiho. Katika salamu hizo, Waziri Mkuu amesema kuwa ...
Marato tv - Sauti ya Jamii