Skip to main content

Posts

Showing posts from April 26, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Prof. Shemdoe Amshukuru Waziri Mkuu Kuadhimisha Miaka 62 ya Muungano kwa Kukagua Miradi, Kutatua Kero za Wananchi

Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amemshukuru  Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba kwa kuadhimisha miaka 62 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukagua ujenzi wa miradi ya maendeleo ya daraja jipya la Mkwajuni, daraja jipya la Kigogo ikiwa ni pamoja na kutatua kero za wananchi wa jiji la Dar es Salaam. Prof. Shemdoe ametoa shukurani hizo leo Aprili 26, 2026 jijini Dar es Salaam       wakati akizungumza na wananchi wa jiji la Dar es Salaam katika Uwanja wa Shule ya Msingi Msimbazi mara baada ya Mhe. Waziri Mkuu kukagua miradi hiyo ya maendeleo, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 62 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. “Mhe. Waziri Mkuu nakushukuru sana kwa uamuzi wako wa kuadhimisha miaka 62 ya Muungano kwa kukagua miradi ya maendeleo na kutatua kero za wananchi wa Dar es Salaam tena siku ya Jumapili,” Prof. Shemdoe amesisitiza. Prof. Shemd...

Waziri Mkuu Ateta na Balozi Wilson Masilingi

 Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amefanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) Balozi Wilson Kajumula Masilingi Ofisi ndogo ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es Salaam, Aprili 27, 2026

Waziri Mkuu Ateta na Balozi Wilson Kajumula

 Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amefanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) Balozi Wilson Kajumula Masilingi Ofisi ndogo ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es Salaam, Aprili 27, 2026.

Makamu wa Rais Ashiriki Usiku wa Mtanzania

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasili katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam, ambapo ni mgeni rasmi katika Hafla ya Usiku wa Mtanzania ikiwa ni shamrashamra za Maadhimisho ya Miaka 62 ya Muungano. Tarehe 26 Aprili 2026.

Wanawake Wahimizwa Kuzingatia Malezi Wanapojikwamua Kiuchumi

Na: Dawati la Habari Polisi Mwanza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu (Jinsia na Wanawake), Felista Mdemu, amewataka wanawake kuhakikisha harakati za kutafuta kipato hazivunji jukumu lao la msingi la malezi ya watoto katika familia. ​Mdemu ametoa wito huo mkoani Mwanza April 25.2026 wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo za "Mwanamke Kinara 2026" kwa Kanda ya Ziwa na Magharibi iliyofanyika katika Ukumbi wa Winter Fell City uliopo Nyasaka, Wilaya ya Ilemela.  Amesisitiza kuwa, pamoja na mwanamke kujiimarisha kiuchumi, ni muhimu kukumbuka kuwa malezi ya watoto ni sehemu ya wajibu wake wa msingi. ​Katika hafla hiyo, jumla ya tuzo 17 zilitolewa, zikiwemo za Mwanamke Mpishi Kinara, Mwanamke Mapambo Kinara, Mwanamke Mwandishi wa Habari Kinara, Madini na Afisa Ustawi wa Jamii Kinara. ​Katika kilele cha tukio hilo, Koplo, Stella Lyimo, ambaye ni Mtendaji wa Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Nyamagana, alinyakua tuzo ya Mwanamke Kinara...

Ubalozi wa Tanzania Washiriki Maonesho ya “culture À L’honneur L’afrique” Jijini Paris

Paris, Ufaransa – 25 Aprili 2026 Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa umeshiriki kikamilifu katika maonesho ya kitamaduni yaliyojulikana kama “Culture à l’Honneur l’Afrique”, yaliyofanyika katika Kituo cha Utamaduni na Kijamii cha Grésillons jijini Paris. Katika maonesho hayo yaliyolenga kuadhimisha na kuenzi tamaduni za Bara la Afrika, banda la Tanzania limejitokeza kuwa moja ya vivutio vikuu, likivutia idadi kubwa ya washiriki na wageni waliopata fursa ya kujifunza kuhusu urithi wa kitamaduni wa Tanzania pamoja na vivutio vyake vya utalii. Wageni waliotembelea banda la Tanzania walipata uzoefu wa kipekee kwa kuvalishwa mavazi ya asili ya Kimasai, hatua iliyoongeza mvuto na uhalisia wa utamaduni wa Kitanzania. Aidha, walipatiwa maelezo ya kina kuhusu vivutio maarufu vya utalii ikiwemo Hifadhi za Taifa, Mlima Kilimanjaro, Fukwe za Zanzibar pamoja na urithi wa kihistoria wa nchi. Watumishi wa Ubalozi walitumia fursa hiyo kusambaza makabrasha mbalimbali ya utalii, k...

Itumieni Zahanati ya Mabatini Mnapougua

Na; Dawati la Habari Polisi Mwanza.  ​Mkuu wa Zahanati ya Polisi Mabatini, mkoani Mwanza, Mrakibu wa Polisi (SP) Daktari Steven Kisaka, amewashauri wakazi wanaoishi karibu na zahanati hiyo iliyopo wilayani Nyamagana, kuitumia kikamilifu kwa ajili ya kupata matibabu wanapougua. ​Daktari Kisaka ametoa ushauri huo Aprili 25, 2026, wakati akishiriki kufanya usafi wa mazingira ya zahanati hiyo na wadau wa maendeleo kutoka kikundi cha "Upendo Federation" cha Kata ya Mabatini, kinachojihusisha na huduma mbalimbali za kijamii. ​Daktari Kisaka, ambaye pia ni Mkuu wa Zahanati hiyo, amesema wataendelea kutoa huduma bora za afya na za uhakika kwa wagonjwa watakaofika kupata matibabu, wakizingatia weledi wa Jeshi la Polisi. ​Mwenyekiti wa kikundi cha Upendo Federation, Seleman Kapera, amesema kuwa wamefika katika zahanati hiyo kufanya usafi kwa kutambua kuwa usafi ni afya, na wataendelea na utaratibu huo katika maeneo mbalimbali. ​Kwa upande wake, Polisi Kata ya Mabatini, Mkaguzi wa Polis...

Dkt. Mwigulu Azungumza na Wakazi wa Dar es Salaam

_Asema Rais Dkt. Samia ni kiongozi mbunifu na wa vitendo_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 26, 2026 anazungumza na wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam ambapo amefanya ziara ya kikazi ya siku moja. Akizungumza katika mkutano wa hadhara unaofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Msimbazi, Dkt. Mwigulu amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kiongozi wa vitendo na mwenye dhamira ya dhati ya kuwatumikia watanzania kwa kutoa majawabu ya changamoto zinazowakabili. Aidha, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa ofisi zote za umma zipo kwa ajili ya kuwatumikia Watanzania kwa kutoa majawabu ya kero za wananchi. Awali Mheshimiwa, Dkt. Mwigulu alikagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mkwajuni lenye urefu wa mita 20 na kimo cha mita 5.5 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 11.6. Pia, Mheshimiwa Waziri Mkuu alikagua mradi wa ujenzi wa Daraja la Kigogo lenye urefu wa mita 50 kimo cha mita 8.9 na barabara unganishi zenye jumla ya urefu wa mita 625 ambalo hadi kuka...