Tume ya Madini kupitia Kurugenzi ya Ukaguzi na Biashara ya Madini imekutana na wadau wa sekta ya madini wakiwemo wachimbaji, wanunuzi na wathaminishaji wa madini, kwa lengo la kupanga bei elekezi za madini ya vito, hatua inayolenga kuimarisha uwiano wa faida, kuongeza mapato ya Serikali na kukuza uchumi wa nchi. Akizungumza jijini Dodoma leo Oktoba 24, 2025, Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini CPA. Venance Kasiki, amesema kikao hicho kimefanyika kwa ajili ya kufanya tathmini na kuweka bei mpya zitakazotumika kwa kipindi cha miezi mitatu, kwa kuzingatia mwenendo wa soko la dunia na gharama halisi za uzalishaji. “Kupitia bei elekezi tunahakikisha wachimbaji, wanunuzi na Serikali wote wananufaika kwa uwiano. Serikali itapata mapato yake kupitia Mrabaha na Ada ya Ukaguzi, huku biashara ikiendelea kwa uwazi na ushindani wa haki,” amesema Kasiki. Amesema hatua hiyo itaimarisha uthabiti wa soko, kuzuia upotevu wa mapato, na kujenga uaminifu kati ya wadau wa sekta ya madini ambayo inac...
Marato tv - Sauti ya Jamii