Mkuu wa Shule ya Mafunzo ya Awali ya Kijeshi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Brigedia Jenerali Sijaona Michael Myalla ameongoza Maafisa na Askari kutoa Misaada ya kibinadamu kwa Jamii ya Kitongoji cha Lukenge kilichopo katika Kijiji cha Kihangaiko Kata ya Msata Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani tarehe 14 Januari 2026. Misaada huo imetolewa kwa wananchi hao ikiwa ni sehemu ya Zoezi la Medani linalojulikana kama EXERCISE MALIZA linalofanywa na kuruti katika eneo la Msata , kwa lengo la kuimarisha mahusiano kati ya Jeshi na wananchi. Katika tukio kulifanyika zoezi la utoaji huduma za tiba na kugawa vyakula kwa wananchi wa kijiji hicho. Akizungumza katika tukio hilo, Mkuu wa Shule ya Mafunzo ya Awali ya Kijeshi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Brigedia Jenerali Sijaona Michael Myalla, amesema zoezi hilo ni sehemu ya kuonesha Umoja na Mshikamano wa Jeshi kwa wananchi wake, sambamba na jukumu la msingi la Ulinzi wa nchi. Brigedia Jenerali Myalla amesisitiza kuwa JWTZ lit...
Marato tv - Sauti ya Jamii