Na Hamida Ramadhan- Dodoma NAIBU Waziri wa TAMISEMI, Dkt.Festo Dugange, amesema mamlaka za serikali za mitaa nchini zinakabiliwa na changamoto nyingi, zikiwemo uhaba wa wataalamu, ukusanyaji mdogo wa mapato, na usimamizi usioridhisha wa miradi ya kimkakati na fedha za umma. Dkt. Dugange ameyasema hayo Desemba 5, 2024, jijini Dodoma, alipomwakilisha Waziri Mohamed Mchengerwa kwenye Mahafali ya 16 ya Chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI) Hombolo. Amebainisha kuwa chuo hicho kina nafasi muhimu katika kusaidia serikali kuzitatua changamoto hizo kupitia utafiti, mafunzo, na ushauri wa kitaalamu. Akiipongeza LGTI Hombolo, Dkt. Dugange amesema chuo hicho kimekuwa kikijenga uwezo wa wataalamu wanaoweza kusaidia serikali kubuni miradi ya kimkakati yenye tija. Amesisitiza kuwa halmashauri zinapaswa kuibua miradi inayoendana na mahitaji ya maeneo yao badala ya kuiga miradi kutoka halmashauri nyingine. Ametoa mfano wa baadhi ya halmashauri kuanzisha miradi ya stendi za mabasi bila kuzingati...
Marato tv - Sauti ya Jamii