Madiwani wa Halmashauri ya Tarime Vijijini Waomba Kutangazwa Tarehe ya Malipo ya Fedha za TASAF Kwa Wahusika
Na Helena Magabe, Tarime Madiwani wa Halmashauri ya Tarime Vijijini wameomba Halmashauri kutangaza siku ya malipo ya fedha za kunusuru Kaya maskini (TASSAF) kama wanavyotangaza Halmashauri ya mji Tarime ili kuepuka pesa kubaki bila kuwafikia walengwa. Hayo waliyasemwa katika kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya mwaka kilichoketi hapo Jana Septemba 3,2024 katika ukumbi wa Halmashauri hiyo ni baada ya kuona miongoni mwa fedha zilizobaki mwaka huu bila kutumika ni pamoja na shilingi bilioni 4,336 ambazo kuzikulipwa kwa walengwa wa mfuko huo. .... Diwani wa Kata ya Kwihancha Ragita Mato ameiomba Halmashauri kuiga mfano wa Halmashauri ya mji Tarime Kwa kutangaza siku ya malipo ya fedha hizo kwenye vituo vyao huku wakisisitiza wapewe fedha zao kwa malipo ya mkononi ili kuepusha usumbufu kwa wale wanaotumia simu za watu kupokea fedha zao. "Kwa nini msiigie mfano wa Halmashauri ya mji Tarime wale wanatangaza siku ya kulipa malipo y...