Wakili wa Rais William Ruto ameanza kwa kusema kuwa anamwakilisha mteja wake na kwamba amesema Mahakama ya Juu haina mamlaka ya kusikiliza na kuamua kesi za kupinga kuondolewa kwa Rigathi Gachagua madarakani zilizowasilishwa. Jopo la majaji watu likiongozwa na Jaji Eric Ogola pia linajumuisha majaji Anthony Mrima na Freda Mugambi lilichanguliwa na Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu kusikiliza kesi zote zenye kuhusiana na kuondolewa madarakani kwa Rigathi Gachagua. Kupitia Wakili Adrian Kamotho, Ruto anadai kuwa Mahakama ya Juu Zaidi pekee ndiyo yenye mamlaka ya kusikiliza kesi hizo. Kulingana na Rais William Ruto, mahakama inafaa kutupilia mbali kesi hizo akidai kuwa zimewasilishwa kinyume cha sheria na ni utumiaji mbaya wa mchakato wa mahakama. Rais Ruto ameongeza kuwa kesi dhidi ya Rais au mtu anayetekeleza majukumu ya afisi ya Rais katika kipindi cha uongozi wake kuhusiana na jambo lolote lililofanywa au kutofanywa chini ya sheria ya Katiba ya Kenya 2010 haziwezi kufunguliwa katika mah...
Marato tv - Sauti ya Jamii