Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amesisitiza umuhimu wa Mkutano wa nchi za Afrika na nchi za Nordic kama jukwaa muhimu la kujadili changamoto zinazokabili Bara la Afrika na kupata suluhu za pamoja kupitia ushirikiano wa kimataifa. Akizungumza katika Mkutano wa 22 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje kati ya nchi za Afrika na nchi tano za Nordic (Denmark, Norway, Sweden, Iceland na Finland), Waziri Kombo alibainisha kuwa migogoro mingi duniani, ikiwemo barani Afrika, imekuwa ikichochewa na masuala ya mipaka, rasilimali, ukosefu wa ajira kwa vijana, tofauti za kikabila na udhaifu wa mifumo ya kuzuia migogoro kabla hazijazuka. Alisisitiza kuwa majukwaa ya kimataifa yana nafasi kubwa ya kusaidia kutatua changamoto hizo kwa kuunganisha nguvu na maarifa ya pamoja. Aidha, alibainisha kuwa msingi wa kudumu wa usalama barani Afrika ni kinga na kuzuia migogoro, badala ya kusubiri izuke. Waziri Kombo pia alieleza kuwa teknolojia na ubunifu ni nye...