WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dkt. Dorothy Gwajima amesema Serikali imeendelea kuimarisha malezi, ulinzi na ustawi wa watoto nchini kupitia programu mbalimbali zinazolenga kujenga kizazi chenye maadili, afya bora na uwezo wa kuchangia maendeleo ya Taifa. Dkt. Gwajima alisema hayo leo Juni 1, 2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Amesema watoto ni rasilimali muhimu na mtaji wa Taifa, hivyo wanapaswa kulelewa katika mazingira salama, yenye upendo na maadili mema ili kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Kwa mujibu wa waziri Gwajima, Amesema Serikali inaendelea kutekeleza Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (2021/22–2025/26), inayolenga kuongeza kiwango cha ukuaji timilifu wa watoto wenye umri chini ya miaka minane kutoka asilimia 47 hadi asilimia 90 ifikapo mwaka 2050. Amesema katika kui...
Marato tv - Sauti ya Jamii