*📌 Dkt. Biteko ahimiza urafiki Nyabionza na Nyuki FC* *📌 Mshindi wa kwanza aibuka na Milioni 6, wapili Milioni 4* Timu ya Nyabiyonza ya Karagwe mkoani Kagera imeibuka kidedea kwa kuifunga mabao mawili kwa moja timu ya Nyuki FC kutoka Bukombe, mkoani Geita katika mechi ya kirafiki iliyofanyika katika Uwanja wa Bashungwa, Karagwe mkoani Kagera. Akizungumza Desemba 20, 2024, Karagwe mkoani Kagera mara baada ya mtanange huo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri na Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewapongeza washiriki wa mechi hiyo na kusema mchezo huo ni sehemu ya kuimarisha umoja, upendo na amani iliyopo. “ Nataka niwahakikishie kuwa watu wa Bukombe watatoka hapa wakiamini ni washindi wa pili, nawapongeza sana makocha wa timu hizi mbili na waamuzi kwa kuamua mpira kwa haki,” amesema Dkt. Biteko. Pia, amewaasa wananchi wa Karagwe kuishi kwa upendo “ Nataka niwasihi watu wa Karagwe kuimarisha umoja wenu kupendana na kuimarisha amani ya wilaya hii,” Pamoja na hayo, Dkt. Biteko ames...