Skip to main content

Posts

Showing posts from March 23, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali Yahimiza Meli ya New Mv Mwanza Kukuza Uchumi, Utalii Kanda ya Ziwa

‎Serikali imetoa wito kwa wafanyabiashara, wasafirishaji na wawekezaji mbalimbali kutumia fursa ya meli mpya ya MV New Mwanza kibiashara na kiutalii ili kukuza uchumi wa Kanda ya Ziwa. Itakumbukwa meli hiyo imejengwa kwa zaidi ya Tsh. Bilioni 120, ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 1,200, tani 400 za mizigo, magari makubwa matatu na madogo, ambapo itafanya safari zake katika bandari zote zinazozunguka Ziwa Victoria ikiwemo Kisumu (Kenya), Port Bay (Uganda) na Kemondo (Bukoba). ‎Akizungumza Jumapili Machi 22, 2026 na waandishi wa habari katika bandari ya Mwanza Kusini jijini Mwanza ilipoegeshwa meli hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Utamaduni ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema kutokana na uwekezaji huo wakazi wa Kanda ya Ziwa, wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa na wadogo wanapaswa kuitumia kwenye shughuli zao na kuleta tija ya uwekezaji huo mkubwa. ‎ ‎Amesema Serikali imetimiza jukumu lake la kutekeleza wajibu wa kujenga mazingi...

Real Admiral Hassan awataka wataalam wa Uokoaji kufanya kazi kwa weledi

Mkuu wa Kamandi ya  Jeshi la Wanamaji Real Admiral  Ameir Ramadani  Hassan amewataka wataalam wa Zimamoto na Uokoaji wa Jeshi la Uinzi la Wananchi (JWTZ) kutekeleza majukumu yao kwa weledi pindi  majanga mbalimbali yanapotokea nchini. Real Admiral Hassan ameyasema hayo wakati akifungua kikao kazi cha wataalam wa Zimamoto na Uokoaji wa JWTZ kilichofanyika katika ukumbi wa Kikosi cha Usafirishaji Mwanza (MTC) tarehe 23 Machi 2026. Amesisitiza kuwa Mafunzo,vifaa na utayari wa kukabiliana na majanga ni jambo muhimu katika kuhakikisha wanakuwa tayari wakati wote pindi majanga yanapotokea Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kukabiliana na  Majanga Kanali Juma Emmanuel Katunge amesema kuwa Makao Makuu ya Jeshi yameandaa kikao hiki ili kuwajengea uwezo wataalam wake na kupata uelewa wa pamoja juu ya majukumu yao. Wataalam wa Zimamoto na Uokoaji jeshini wamekua wakishiriki katika operesheni za uokozi katika majanga ya asili na ajali mbalimbali kwa kusaidiana na Mamlaka nyingin...

Cheti cha Polisi Chafungua Ukurasa Mpya Kwa Harbinder Singh Sethi

  Na Prosper Makene  JESHI la Polisi Tanzania limetoa cheti cha kumsafisha Mwenyekiti wa Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Harbinder Singh Sethi dhidi ya uhalifu katika kumbukumbu zao. Cheti cha Kibali cha Polisi chenye kumbukumbu namba FB/FP/G.4/2026/VOL.III/49198, kimetolewa na Ofisi ya Uchunguzi wa alama za vidole na Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam. Cheti hicho kimekuja baada ya Mwenyekiti wa IPTL, Harbinder Singh Sethi kuachiliwa na mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu baada ya kukaa mahabusu kwa zaidi ya miaka minne kwenye kesi ya uhujumu uchumi, na cheti hicho kinaonyesha na kuthibitisha wa msimamo wake, na kuthibitisha kuwa hana hatia katika mashitaka aliyowahi kushitakiwa nayo. Mwenyekiti huyo wa IPTL alikamatwa wakati wa utawala wa Magufuli huku kukiwa na tuhuma za uhujumi uchumi unaohusishwa na uendeshaji wa IPTL. Ofisi ya Uchunguzi ilishughulikia upekuzi wa alama za vidole vya Harbinder ili kuthibitisha kama alikuwa na hatia yoyote iliyosajiliw...

Tanzania: Police Certificate Confirms Harbinder Sethi's Clean Record

By Prosper Makene  The Tanzania Police Force has issued a certificate to clear Harbinder Singh Sethi, Chairman of Independent Power Tanzania Limited (IPTL), of any criminal antecedents in their records. The Police Clearance Certificate with reference number FB/FP/G.4/2026/VOL.III/49198, was issued by the Forensic Bureau of the Tanzania Police Force in Dar es Salaam. The certificate came after IPTL chairman Harbinder Singh Sethi was released by the court after spending over four years behind bars on an economic sabotage case, and this clearance is seen as a vindication of his stance, proving he has clean hands. The IPTL chairman was arrested during the Magufuli regime amid allegations of economic crimes tied to IPTL's operations. The Forensic Bureau processed Harbinder's fingerprint search to verify if he had any registered convictions in Tanzania. Officials at the bureau took Harbinder's fingerprints to conduct a thorough investigation for criminal records. The search invol...

Wizara Maji na matumizi ya teknolojia katika utatuzi wa changamoto

Na: Dk. Reubeni Lumbagala  Wiki ya Maji Kitaifa nchini Tanzania na Siku ya Maji Duniani imemalizika Machi 22, 2026. Imekuwa ni wiki nzuri kwani mijadala mbalimbali yenye tija kuhusiana na sekta ya maji imefanyika kwa mafanikio makubwa. Kutokana na umuhimu wa maji, serikali, mashirika, asasi na wananchi kwa ujumla katika Siku ya Maji Duniani, hujadili masuala mbalimbali yahusuyo sekta ya maji kwa maendeleo. Kimsingi, mijadala ya kuangazia mafanikio na changamoto za sekta ya maji inafanyika kwa madhumuni ya kuboresha hali ya usambazaji wa maji kwa wananchi na kuangalia namna maji yatakavyosaidia sekta nyingine kama kilimo, viwanda, mifugo, uvuvi, nishati, kutaja kwa uchache katika kukuza uchumi kwa maendeleo endelevu. Wizara ya Maji imefanikiwa katika maeneo mengi. Mathalani, suala la usambazaji wa maji kwa wananchi ambapo maeneo ya mijini usambazaji wa maji umefikia asilimia 92.5 na vijijini asilimia 85.2. Wizara ya Maji imefanikiwa pia kutekeleza miradi mingi kama Mradi wa Miji 28....

Maboresho mfumo kodi na maendeleo tuyatakayo

Na: Dk. Reubeni Lumbagala, Tanga  Juhudi za kujiletea maendeleo zinategemea sana ufanisi wa ukusanyaji kodi kutoka kwa wananchi. Wizara, taasisi na vitengo mbalimbali wanaweza wakakaa chini kupanga, kujadili na kuja na mipango mingi mizuri ya maendeleo lakini itakapofika kipengele cha namna ya kutekeleza mipango hiyo, maeneo mengi yatahitaji fedha ili kufanikisha. Kimsingi, kodi ni raslimali muhimu inayowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambayo ni muhimu katika kufikia maendeleo ya kweli yanayohusa maisha ya wananchi kule walipo. Hakuna namna serikali inaweza kuwaletea maendeleo wananchi wake pasipo kukusanya kodi. Kivipi? Mathalani, wananchi wanahitaji kujengewa barabara, madaraja, shule, masoko, hospitali au wanahitaji dawa hospitalini, vitendea kazi katika ofisi za umma na mengine kadha wa kadha; sasa,  ili serikali ifanikishe mahitaji hayo ya wananchi, ni lazima fedha zitumike kununua mahitaji yote muhimu kufanikisha ujenzi na ununuzi wa vifaa mbalimbali, yaani ni ...

Ushiriki wa Watanzania Sekta ya Madini Waongezwa Kupitia Huduma za Kisheria

📍 Dodoma, Machi 23, 2026 Serikali kupitia Tume ya Madini imeendelea kusisitiza umuhimu wa utekelezaji madhubuti wa sheria na kanuni katika sekta ya madini, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha rasilimali za taifa zinawanufaisha Watanzania na kulinda maslahi mapana ya nchi. Akizungumza jijini Dodoma katika kikao kazi kilichowakutanisha wawakilishi wa mawakili kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Ofisi ya Mwasheria Mkuu wa Serikali pamoja na viongozi kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na taasisi ya Breakthrough Attorneys, Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini, CPA Venance Kasiki, amesema wanasheria na kampuni za sheria ni wadau muhimu katika kuimarisha ufuataji wa sheria na utatuzi wa migogoro katika sekta hiyo. Amesema uwepo wa ushauri bora wa kisheria unachangia kuongeza ufanisi wa shughuli za uchimbaji, hususan kwa wamiliki wa leseni, wakandarasi na watoa huduma migodini, hivyo kuchochea ukuaji endelevu wa sekta ya madini. CPA Kasiki amefafanua kuwa kikao hicho kim...

Waomba huduma ya kipolisi irejee, RPC Mutafungwa awataka kutunza amani

​*Kutoka: Dawati la Habari Polisi Mwanza* Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza ameridhia ombi la wananchi wa Kata za Mabatini na Mbugani, Wilaya ya Nyamagana, la kurejesha huduma za kipolisi katika Kituo cha Polisi Mabatini kilichoharibiwa wakati wa vurugu za Oktoba 2025. ​Hayo yamejiri wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika tarehe 22.03.2026 katika uwanja wa Shule ya Msingi Mabatini "B", uliowakutanisha wananchi wa kata hizo mbili na Jeshi la Polisi. ​Akizungumza na wananchi kupitia mkutano huo, Kamanda alisema amesikia kilio chao cha muda mrefu na akawahakikishia kurejesha huduma hiyo, kwa kuwa wananchi wenyewe wameamua kukikarabati kituo hicho kilichoharibiwa na kuchomwa moto. ​Aidha, Kamanda alisema wananchi wanatakiwa kutambua kuwa jukumu la kuzuia uhalifu si la Jeshi la Polisi pekee, wala si la viongozi wa Serikali za Mitaa peke yao, bali ni jukumu la wananchi wote kwa sababu wahalifu wanatoka miongoni mwa jamii. Alisisitiza kuwa watawadhibiti wahalifu kwa kukataa uhalifu...