Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka Nchini Kenya (IEBC) imetangaza kuwa chaguzi ndogo 24 zinazosubiriwa kwa muda mrefu zitafanyika Novemba, 27 2025, na hivyo kumaliza miezi ya ukosefu wa uwakilishi katika maeneo husika. Katika taarifa iliyotolewa Jumamosi, IEBC ilisema uchaguzi huo mdogo utafanyika kwa awamu mbili, ambazo zitachapishwa katika gazeti rasmi la serikali mwezi huu. Hali hii imefungua uwanja wa mapambano ya kisiasa yanayotarajiwa kuhusisha Rais William Ruto, kiongozi wa ODM Raila Odinga, na aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ambaye sasa anaongoza muungano mpya wa upinzani. Awamu ya kwanza ya tangazo hilo, iliyochapishwa Ijumaa Agosti 8, inahusisha Wadi 16 katika kaunti 12, zikiwemo Angata Nanyokie (Samburu), Chemundu/Kapng’etuny (Nandi), Chewani (Tana River), Fafi (Garissa), Kariobangi North (Nairobi), Kisa East (Kakamega), Metkei (Elgeyo Marakwet), Mumbuni North (Machakos), Narok Town (Narok), Purko (Kajiado), Tembelio (Uasin Gishu), Nyansiongo, Nyamaiya, na Eke...