Skip to main content

Posts

Showing posts from May 3, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Makonda: Kiswahili kupaa Kidijitali, Serikali yalenga Maneno Millioni 100 katika Kokita

  WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, leo Mei 4, 2026, akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo, amesema Serikali imejipanga kuifanya lugha ya Kiswahili kuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya teknolojia duniani. Akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo leo Mei 4,2026, Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Poul Makonda amesema Kupitia Baraza la Kiswahili la Taifa, Serikali imeanzisha Kongoo ya Kiswahili ya Taifa (KOKITA), mradi mkubwa unaolenga kukusanya na kuhifadhi msamiati wa Kiswahili kwa matumizi ya kidijitali. “Tunataka Kiswahili kisiwe nyuma katika mapinduzi ya teknolojia; KOKITA ni daraja la kukipeleka katika matumizi ya Akili Unde (AI),” amesema Makonda. Ameeleza kuwa kuanzia Julai 2025 hadi Aprili 2026, jumla ya maneno milioni 22 yameingizwa kwenye kongoo hiyo, na kufikisha maneno milioni 61, huku lengo likiwa kufikia maneno milioni 100. Aidha, ushirikiano unaendelea kuimarishwa na taasisi kama Mozilla Foundation ili k...

Toeni Huduma za afya Kwa Kuzingatia Utu,Maadili

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka viongozi na watumishi wa sekta ya afya kuzingatia kutoa huduma za staha, utu na huruma kwa wananchi na kufuata maadili ya kada zao Waziri *Mchengerwa ameyasema hayo leo Mei 3, 2026, jijini Mwanza wakati akifungua kikao kazi cha Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Wizara ya Afya* Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya *Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan* imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika kuboresha miundombinu ya afya nchini, ikiwa ni pamoja na ununuzi wa *mashine za kisasa kama MRI, CT-Scan na vifaa vya kusafisha figo pamoja na ukarabati wa vituo vya kutolea huduma.* “Uwepo wa majengo mazuri na vifaa vya kisasa hauwezi kuwa na maana endapo huduma zinazotolewa hazina utu na huruma kwa wagonjwa,” amesema Mhe. Mchengerwa  *Mhe. Mchengerwa* ameongeza kuwa lugha chafu, rushwa, upendeleo na uzembe vinaweza kufuta kabisa thamani ya uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika kuboresha sekta hiyo muhimu. Aidha, Mhe. *Mchengerwa amewat...

Massaburi Aongoza Harambee ya Kanisa Kivule

KATIKA kuendeleza mshikamano wa kijamii na kuunga mkono juhudi za maendeleo ya kiroho, Mbunge wa Jimbo la Kivule, Ojambi Massaburi, kupitia Katibu wake Wakili Msomi Mashaka Nyadhi, ameongoza harambee ya uchangiaji kwa ajili ya ununuzi wa eneo la Kanisa la E.A.G.T Lango la Rehema, lililopo Mtaa wa Magole A, Kata ya Kivule, Mei 3, 2026. Harambee hiyo imekuwa na mafanikio makubwa baada ya kufanikisha kukusanya jumla ya shilingi 8,448,000, fedha zitakazosaidia kutimiza azma ya kanisa hilo kupata eneo lake rasmi na kuimarisha huduma za kiroho kwa waumini. Akihutubia waumini na wananchi waliojitokeza kushiriki tukio hilo, Nyadhi aligusia nguvu ya umoja na umuhimu wa kujitolea kwa maendeleo ya jamii. “Ushirikiano wetu ndio msingi wa mafanikio ya kweli. Tunapoweka nguvu pamoja, hakuna linaloshindikana ,haya ndiyo maendeleo tunayoyahitaji katika jamii yetu,” alisisitiza. Aidha, aliwahamasisha kuendeleza moyo wa kuchangia na kushirikiana, akibainisha kuwa uwekezaji katika taasisi za kijamii na k...

Rais Ruto kuwasili Leo mei 4,2026 Kwa ziara ya kihistoria ya siku mbili

RAIS wa Jamhuri ya Kenya, William Samoei Ruto, anatarajiwa kuwasili nchini Tanzania leo Mei 4, 2026, kwa ziara ya kitaifa ya siku mbili yenye lengo la kuimarisha uhusiano wa kimkakati kati ya Kenya na Tanzania. Akiwa nchini, Rais Ruto atafanya mazungumzo ya ana kwa ana na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kabla ya kuongoza mazungumzo rasmi yatakayojumuisha ujumbe wa nchi zote mbili.  Viongozi hao pia watazungumza na waandishi wa habari kuhusu maazimio ya kikao hicho ambapo Mazungumzo hayo yanatarajiwa kujikita katika kuimarisha ushirikiano wa kindugu na kiuchumi, hususan katika sekta za biashara, uwekezaji, miundombinu na usafirishaji, pamoja na kufungua fursa mpya za maendeleo kwa pande zote mbili. Katika hatua nyingine muhimu, viongozi hao watashuhudia utiaji saini wa hati mbalimbali za makubaliano na mikataba ya ushirikiano, sambamba na kushiriki Jukwaa la Biashara litakalowakutanisha wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Tanzania na Ken...

Rais Samia akimpokea mgeni wake Rais wa Rwanda

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Matukio tofauti ya picha alipompokea mgeni wake Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame alipowasili Ikulu ya Dar es salaam leo Mei 03, 2026.

Rais Kagame atua Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame amewasili nchini kwa Ziara ya Kikazi ya siku moja yenye lengo la kuimarisha uhusiano wa uwili kati ya Tanzania na Rwanda. Mhe. Rais Kagame anatarajia kukutana na kufanya mazungumzo  na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu jijini Dar es Salaam. Inategemewa kwamba Ziara hii itadumisha mahusiano mazuri na ya kihistoria kati ya majirani hawa wawili. Ushirikiano huu umezidi kuimarika katika miaka ya hivi karibuni kwa kupitia Tume ya Kudumu ya Pamoja (JPC), ambapo Tanzania imeendelea kuwa miongoni mwa washirika wakuu watatu wa biashara wa Rwanda duniani, huku kiwango cha biashara kati ya nchi hizi kikiongezeka kila mwaka.  Aidha, katika uwekezaji, kuanzia mwaka 1990 hadi Machi 2026, Tanzania imesajili miradi 42 ya uwekezaji kutoka Rwanda yenye thamani ya dola za Marekani milioni 325.53 na kuunda ajira 2,225 katika sekta mbalimbali ikiwemo viwanda, usafirishaji, huduma za kifedha, mali...