MBUNGE wa Jimbo la Kasulu Vijijini Edibilly Kazala amesema Tanzania inapaswa kuchukua hatua za haraka kuvilinda viwanda vya ndani na kukuza uwekezaji wenye tija, akionya kuwa sekta ya viwanda vya nguo nchini inaendelea kudorora kwa kasi. Akizungumza na waandishi wa habari katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma jana Mei 22, 2026, Kazala amesema pamoja na ongezeko la wawekezaji wa kigeni nchini, bado kuna baadhi ya uwekezaji mdogo usio na manufaa makubwa kwa Taifa huku ukichukua nafasi ambazo Watanzania wana uwezo wa kuzifanya wenyewe. “Lazima kama Taifa tuangalie namna ya kudhibiti baadhi ya uwekezaji usio na tija kubwa kwa wananchi wetu,” amesema. Kazala amesema takwimu za ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) zinaonyesha kuwa mwaka 2002 Tanzania ilikuwa na zaidi ya viwanda 50 vya nguo, lakini sasa vimebaki takribani vitatu pekee vinavyoendelea kufanya kazi, hali inayodhihirisha kuporomoka kwa sekta hiyo muhimu. Amesema kushuka kwa sekta ya textile kumeathiri pia ajira, ambapo mwaka 2015 sek...
Marato tv - Sauti ya Jamii