Skip to main content

Posts

Showing posts from April 24, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Serikali Yaimarisha Uwazi Sekta ya Madini, Bei Elekezi Kutolewa Kila Siku

KAHAMA Serikali kupitia Tume ya Madini imesema itaendelea kutoa bei elekezi za madini ya dhahabu, shaba na fedha kila siku itakayotumika kwenye masoko na vituo vya ununuzi wa madini hatua inayolenga kuongeza uwazi katika biashara ya madini na kuwawezesha wachimbaji kuuza madini yao kwa bei halisi ya soko la dunia. Akifunga mafunzo kwa Mameneja na Wakaguzi Wakuu wa Migodi ya uchimbaji mdogo kutoka mikoa ya kimadini ya Kahama, Mbogwe na Shinyanga mapema jana, Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini, CPA Venance Kasiki alisema taarifa hizo za bei zitawasaidia wachimbaji kufanya maamuzi sahihi ya biashara na kuepuka hasara zitokanazo na madalali maarufu kama vishoka. Alisema hapo awali baadhi ya wachimbaji walikuwa wakiuza madini bila kufahamu bei halisi ya soko la dunia, hali iliyosababisha kupoteza mapato na kuingia katika mikataba isiyo na manufaa.  Alifafanua kuwa kwa sasa bei za madini hutolewa kila siku, hivyo mchimbaji ana uwezo wa kufanya uamuzi sahihi kabla ya kuuza madini...

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Jkt Amtembelea Mama Maria Nyerere

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Mhe.Dkt.Rhimo Nyansaho (Mb) , tarehe 24, April 2026, Amemtembelea na kumjulia hali Mama Maria Nyerere Nyumbani kwake Msasani jijini Dar-es-salaam.  Katika ziara hiyo Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na JKT Dkt.Rhimo Nyansaho alipata fursa ya kukutana pia na familia nzima ya Marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarege Nyerere. Akiwa Msasani Waziri wa Ulinzi na JKT alipata fursa ya Kujadiliana mambo mbalimbali na Mama Maria Nyerere na akatumia fursa hiyo kumshukuru Mama Maria kwa mchango mkubwa wa Baba wa Taifa , Mwalimu Nyerere alioutoa kwa Taifa na Afrika kwa ujumla. Waziri Nyansaho akamuahidi Mama Maria Nyerere kuwa Serikali ya Rais Dkt  Samia Suluhu Hassan na Watanzania kwa ujumla wataendelea kumuenzi Mwalimu Nyerere daima Aidha Mhe.Dkt.Rhimo Nyansaho pamoja na kukutana na Mama Maria alipata fursa ya kukutana na wanafamilia wa Baba wa Taifa akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mheshimiwa Makongoro Nyerere ambaye ni Mtoto wa tano wa Mwalimu ...

Wakaguzi Wakuu wa Migodi Watakiwa Kuwa Mabalozi wa Biashara Halali ya Madini

📍KAHAMA Serikali imewataka Wakaguzi Wakuu wa Migodi pamoja na Mameneja wa Migodi nchini kuwa mabalozi wa utekelezaji wa sheria, kanuni za madini na kuwa wazalendo katika biashara ya madini ili kuongeza mchango wa sekta hiyo kwenye uchumi wa taifa. Wito huo umetolewa leo Aprili 24, 2026 wilayani Kahama, mkoani Shinyanga na Mtaalam kutoka Kurugenzi ya Ukaguzi na Biashara ya Madini  Tume ya Madini, Mhandisi Erasmina Massawe, kwenye mafunzo kwa Mameneja na Wakaguzi Wakuu wa Migodi ya uchimbaji mdogo yaliyowakutanisha washiriki kutoka mikoa ya kimadini ya Kahama, Mbogwe na Shinyanga. Mafunzo hayo yamelenga kuimarisha uelewa wa kitaalam, usimamizi bora wa migodi, uzingatiaji wa sheria na kanuni za madini pamoja na kukuza uchimbaji salama na endelevu. Amesema mbali na kujifunza mbinu za kuimarisha usalama migodini, viongozi hao wanapaswa kuwa sehemu ya mikakati ya Serikali ya kuhakikisha biashara ya madini inafanyika kwa uwazi na kwa kuzingatia Sheria ya Madini na kanuni zake, hatua itak...

Wananchi Chunya Kunufaika na Mradi wa Majiko Banifu kwa Bei ya Ruzuku.*

  📌 *Majiko 1,555 kuuzwa kwa bei ya ruzuku*  📌 *Serikali kutoa ruzuku ya asilimia 85 kwa kila jiko* . 📍 *Chunya, Mbeya*  Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa halmashauri hiyo, Wakili Athumani Bamba leo Aprili 24, 2026 amezindua rasmi mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku katika mji mdogo wa Makongolosi, wilayani Chunya mkoani Mbeya. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mradi huo unalenga kuwapatia wananchi nishati mbadala iliyo nafuu, salama na rafiki kwa mazingira, huku ukichochea kupunguza matumizi makubwa ya kuni na mkaa ambao umeendelea kuwa chanzo cha uharibifu wa misitu. Alieleza kuwa kupitia mpango huo wa ruzuku, wananchi wataweza kumudu kununua majiko banifu kwa gharama nafuu zaidi, jambo litakalosaidia kupunguza matumizi ya nishati zisizo rafiki pamoja na kuboresha afya za watumiaji kwa kupunguza athari za moshi majumbani. “Ni muhimu wananchi wakautum...