Skip to main content

Posts

Showing posts from June 10, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Diwani Njofu Aanika Mafanikio Ya Uongozi Wake Kipindi Cha Mwaka Mmoja

Na Shomari Binda-Musoma  DIWANI wa Kata ya Mahikamano Njofu Constantine Katama ameanika mafanikio yaliyopatikana kwa kipindi cha uongozi wake kwa mwaka mmoja. Akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi(CCM) ya 2020/2025 leo juni 11,2025 wakati wa ziara ya mbunge wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo. Amesema katika kipindi cha mwaka 2024/2025 wa uongozi wake amewawakilusha vyema wananchi katika usimamizi rasilimali na Sheria ndani ya Halmashauri. Njofu amesema kama diwani amefanikiwa kuwawezesha vijana,wanawake na wenye ulemavu kupata mikopo isiyo na riba kutoka halmashauri. Amesema ndani ya kipindi hicho licha ya uwezeshaji wananchi kiuchumi kupitia mikopo hiyo yapo ya kimaendeleo ambayo yamefanyika kwenye sekta ya elimu,afya,maji,miundombinu na mambo mengine. Diwani huyo ambaye alichaguliwa mwezi machi 2024 kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa Kata hiyo Charles Mwita kwenye kipindi cha uongozi wake ameweza pia kuhamasisha wananchi matumizi ya ...

Askari 238 Wahitimu Mafunzo Jeshi La Uhifadhi

*Na. Happiness Sam- Katavi* Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anayeshughulikia masuala ya Uhifadhi Kamishna wa Polisi (CP) Benedict Wakulyamba,Jana Juni 10, 2025 amefunga rasmi mafunzo kwa Maafisa na Askari wapya 238 wa Jeshi la Uhifadhi na Misitu kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) katika Kituo Cha Mafunzo cha Jeshi hilo kilichopo Mlele mkoani Katavi. Akizungumza wakati wa kuhitimisha mafunzo hayo CP Wakulyamba alisema, “mafunzo haya mliyoyapata ni muhimu kuyatekeleza kwa vitendo pamoja na kuwa na ushirikiano mzuri kazini kwa lengo la kuboresha utendaji  kazi na kuyaishi yale  yote mliyofundishwa ili kuchochea uwajibikaji”. Aidha, CP Wakulyamba alieleza kuwa mafunzo hayo hayawezi kuwa na maana yoyote endapo yatabaki kama nadharia isiyofanyiwa kazi, bali ni lazima yatumiwe kama nyenzo ya kuchochea uwajibikaji, maadili mema, na nidhamu kazini na kuwataka wahitimu wa mafunzo hayo kuwa mfano bora wa kuigwa katika maeneo yao ya kazi kwa kutumia maari...

Makamu wa Rais Asisitiza Mshikamano Kimataifa

  Na Mwandishi wetu Jovina Massano. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito kwa Mataifa kuhakikisha kunakuwa na hatua za pamoja, kuwepo mshikamano wa kimataifa, na uwekezaji endelevu ili kuhakikisha uchumi endelevu wa bahari, kupunguza uchafuzi wa mazingira pamona na kulinda bioanuwai ya baharini.  Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akihutubia Mkutano wa Tatu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Bahari (UNOC3) akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano huo unaofanyika Jijini Nice nchini Ufaransa.  Amesema hapana budi kuwa na hatua za ujasiri zikazoratibiwa kwa ufanisi ili kuhakikisha maendeleo makubwa katika uendelevu wa bahari na ni muhimu kuongeza ufadhili katika kushughulikia changamoto za bahari, kwa kuzingatia zaidi kusaidia nchi za kipato cha chini na nchi zinazoendelea za Visiwa Vidogo, ambazo zinakabiliwa na ufinyu wa bajeti na mizigo ya madeni inayokwamisha kufikia ahad...

Nirc Yaendelea na Utelekelaji wa Ahadi ya Rais Samia Kuchimba Visima 67,000 Vya Umwagiliaji,Nchi Nzima

 📍NIRC; Dodoma   Serikali ya Awamu ya Sita,  kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, imeanza utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya uchimbaji wa visima virefu 67,000 vya maji kwa ajili ya kiliko cha Umwagiliaji nchini. Lengo ni kuhakikisha kuwa Taifa linaondokana na kilimo cha kutegemea mvua na kuwa na uhakika wa maji kwa ajili ya kilimo na kulima zaidi ya mara moja kwa mwaka Hatua hiyo imetokana na ahadi ya Rais Dkt.Samia, aliyoitoa wakati wa maazimisho ya siku ya Wakulima Duniani( Nane Nane), yaliyofanyika kitaifa jijini Mbeya, mwaka 2023. Hayo yamesemwa leo  jijini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Bwana Raymond Mndolwa, wakati wa kuanza kwa zoezi la uchimbaji wa visima kwa kutumia mitambo iliyonunuliwa na Serikali katika mashamba ya BBT (Chinangali) ya programu ya  *Jenga Kesho iliyo Bora* (BBT), inayowawezesha vijana kujiajiri katika kilimo. Mndolwa amesema Serikali ya Dr. Samia imeiwezesha Tume kununua...

Mbunge Mathayo Aanza Ziara Usomaji Ilani Kata Kwa Kata Kwa Kishindo

Na Shomari Binda-Musoma  MBUNGE wa Jimbo la Musoma Mjini Vedastus Mathayo leo juni 10,2025 ameanza ziara ya siku 4 Kata kwa Kata kusoma utekelezaji wa ilani Kishindo cha mbunge huyo kimeanzia Kata ya Rwamlimi,Bweri,Kitaji na kunalizia Nyakato ambako kote amepata mapokezi makubwa. Akiwa kituo cha kwanza Kata ya Rwamlimi wajumbe wa Mkutano Mkuu waliohudhuria kikao hicho wameguswa na utendaji kazi na utekelezaji wa ilani uliofanywa na mbunge huyo na kuamua kumchangia fedha za kuchukua fomu kugombea tena nafasi hiyo. Wakizungumza na GMTV wajumbe hao wamesema yaliyofanywa na mbunge huyo chini ya Dkt.Samia Suluhu Hassan Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho hawana budi kumuunga mkono tena. Wamesema kwenye sekta moja tu ya elimu ni mambo makubwa yamefanyika lakini kwa mbunge hadi sasa anaendelea na utengenezaji wa madawati,viti na meza kwaajili ya shule za msingi na sekondari na tayari vifaa hivyo vimeshafikishwa mashuleni. Wajumbe hao wamesema hakuna mwananchi aliyechangishwa fedha kwenye u...

Chadema Yawekwa Gerezani Hadi Kesi ya Msingi Kutolewa Uamuzi

 Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimezuiwa kufanya shughuli zozote zile za kichama na Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam. Zuio hilo linatokana na kesi namba 8323/2025 iliyofunguliwa na aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar, Said Issa na wenzake wawili ambayo imetolewa uamuzi leo na Jaji Hamidu Mwanga. Uamuzi huo umetolewa huku CHADEMA ikikosa muwakilishi wa kisheria baada ya Wakili Jebrah Kambole aliyekuwa akisimamia kesi hiyo kujitoa kabla ya kutolewa uamuzi akidai kutosikilizwa kwa hoja zao. Hatua ya CHADEMA kuzuiwa kufanya shughuli hizo inatokana na maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na jopo la Mawakili wa walalamikaji ya kwamba liwekwe zuio hilo hadi kesi ya msingi itakapotolewa uamuzi. Kesi hiyo itaanza kusilizwa Juni 24, 2025 na Mbali na Mohammed, wengine ni Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa chama hicho, Ahmed Rashid Khamis na Maulida Anna Komu wanaojitambulisha kama wajumbe wa bodi ya wadhamini. Katika kesi hiyo ya madai na...

Chadema Marufuku Kufanya shughuli za Kichama kwa Muda wa Siku 14

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimezuiwa kwa siku 14 kufanya shughuli zozote zile za kichama na Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam.  Zuio hilo linatokana na kesi namba 8323/2025 iliyofunguliwa na aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar, Said Issa na wenzake wawili ambayo imetolewa uamuzi leo na Jaji Hamidu Mwanga. Uamuzi huo umetolewa huku CHADEMA ikikosa muwakilishi wa kisheria baada ya Wakili Jebrah Kambole aliyekuwa akisimamia kesi hiyo kujitoa kabla ya kutolewa uamuzi akidai kutosikilizwa kwa hoja zao.  Hatua ya CHADEMA kuzuiwa kufanya shughuli hizo inatokana na maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na jopo la Mawakili wa walalamikaji ya kwamba liwekwe zuio hilo hadi kesi ya msingi itakapoanza kusikilizwa Juni 24, 2025.  Mbali na Mohammed, wengine ni Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa chama hicho, Ahmed Rashid Khamis na Maulida Anna Komu wanaojitambulisha kama wajumbe wa bodi ya wadhamini.  Katika kesi hiyo ya madai nam...

MwanaFA: Sasa nitalala usingizi baada ya kupatikana kituo cha afya tarafa ya Amani

📌 Zabuni ya ujenzi wa kituo hicho kutangazwa Jumatatu Na Mwandishi Wetu, Muheza  NAIBU Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Hamisi Mwinjuma maarufu MwanaFA, amesema kukosekana kwa kituo cha afya tarafa ya Amani kulikuwa kukimkosesha usingizi kwa kuwa hakutaka miaka yake mitano ya awali ya ubunge asimalize bila kupatikana kituo hicho. Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi kiasi cha shilingi milioni 645.2 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kituo hicho iliyofanyika katika eneo litakalojengwa  kwenye zahanati ya Kijiji cha Mgambo Miembeni, alisema suala la kituo lilitolewa ahadi na wabunge waliopita tangu mwaka 1998. Alisema kituo hicho kilikuwa na siasa kubwa kutoka kwa watangulizi wake wa nafasi hiyo, hivyo kupatikana kwa kituo hicho ni faraja kwake na Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya wabunge waliopita kutoa ahadi bila mafanikio. "Nimewahi kuja Amani mara nyingi sana lakini leo, nimekuja kama kidume kweli kweli, mara hii nimekuja Kifua mbele kama nimepigwa ngumi ya mgo...