Tanzania imesisitiza umuhimu wa kukuza ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji na nchi marafiki, ikiamini kuwa hiyo ndiyo njia bora zaidi ya kukuza uchumi kwa manufaa ya wananchi. Kauli hiyo imetolewa Oktoba 09, 2024 jijini Helsinki, Finland na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo wakati anashiriki kikao cha Mashauriano ya Kisiasa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Finland, Mhe. Elina Valtonen na Naibu Mawaziri wa Wizara hiyo, Mhe. Pasi Hellman anayeshughulikia masuala ya Maendeleo ya Kimataifa na Mhe. Jarno Syrjälä anayeshughulikia Biashara za Kimataifa. Waziri Kombo amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya mabadiliko makubwa ya mifumo ya sera na sheria ili kuboresha mazingira ya biashara kwa lengo la kuvutia uwekezaji nchini Tanzania. Hivyo, ametoa wito kwa wawekezaji wenye mitaji na dhamira ya dhati ya kuwekeza, waondoe hofu kuhusu Tanzania, kwani nchi hiyo ni mahali salama kwa waweke...
Marato tv - Sauti ya Jamii