Na Sixmund Begashe - Serengeti Ziara ya kikazi ya watafiti wa mimea vamizi kutoka Jamhuri ya Cuba walioungana na wataalam wa ikolojia kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii katika Hifadhi ya Taifa Serengeti inatarajiwa kuwa neema kubwa kwa Wanyamapori kwenye Hifadhi hiyo, kwa kuongeza maeneo ya malisho kwa wanyama hao ambayo kwa sasa yameanza kuathiriwa na mimea vamizi. Akizungumza na watafiti hao katika Hifadhi hiyo ya kipekee duniani, Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Serengeti, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Stephano Msumi ameushukuru na kuupongeza uongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa hatua hiyo muhimu ya kuwakutanisha watafiti wa Wizara hiyo na kutoka nchi Cuba kutembelea Hifadhi ya Serengeti ili kujionea changamoto hiyo kwa lengo la kutafuta ufumbuzi wakudumu. Aidha, amesema kuwa Hifadhi hiyo ni moja ya Hifadhi za Taifa zinazochangia kwa kiasi kikubwa katika pato la taifa kupitia utalii hususani wa Wanyamapori hivyo jitihada zinazofanywa na Serikali katika kuhaki...
Marato tv - Sauti ya Jamii