Skip to main content

Posts

Showing posts from January 13, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waandishi na wachapishaji vitabu kukutana kesho Dar

Na Mwandishi Wetu BODI ya Huduma za Maktaba Tanzania (TLSB), imeandaa mkutano wa waandishi na wachapishaji wa vitabu kuhusu Sheria ya amana kwenye maktaba mtandao wa taifa na ununuzi wa vitabu kwa ukuzaji wa soko la ndani utakaofanyika kesho. Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya  Wakurugenzi  ya (TLSB), Profesa Rwekaza Mukandara. Mkurugenzi Mkuu wa (TLSB), Dk. Mboni Ruzegea, alisema jana kuwa mkutano huo utafanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa TLSB Maktaba Kuu ya Taifa na kwamba lengo ni kujadili kwa pamoja utekelezaji wa sheria ya amana katika mfumo wa maktaba mtandao wa taifa na ununuzi wa vitabu kutoka kwa waandishi na wachapishaji wa ndani. Alisema TLSB iliyoanzishwa kwa Sheria ya mwaka 1975 inawapa mamlaka ya kuendeleza masuala ya maktaba kwa kuhakikisha nchi inakuwa na vitabu vya kutosha kupitia maktaba. “Mkutano huu  wa kesho unalenga tunachofanya kila siku kwa hiyo tunataka kuzungumza na wachapishaji na wazalishaji  kuhusu ubora wa wanachozalish...

Rais Samia afanya Mazungumzo na Viongozi Mbalimbali Ikulu Dar Es Salaam

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Bi. Susan Namondo, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Januari, 2025. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Balozi wa Japan hapa nchini anayemaliza muda wake Mhe. Yasushi Misawa, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Januari, 2025. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Tanzania Bi. Ruth Zaipuna Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Januari, 2025.

Dc Sima-Tutachukua hatua kwa Wakuu wa Shule watakaoweka Vikwazo kwa Watoto

 Angela Sebastian; Bukoba Mkuu wa wilaya ya Bukoba mkoani Kagera Erasto Sima amewataka walimu wakuu na wakuu wa shule za msingi na sekondari kutowawekea vikwazo wanafunzi wanaoripoti shuleni. Aidha Sima amewataka wazazi kutotumia nafasi hiyo kushindwa kutimiza wajibu wao wa kuwapatia watoto wao mahitaji muhimu ya shule ikiwemo sare,viatu na madaftari wakisingizia kusamehewa na Serikali. "Tuwavumilie wanafunzi wanaoripoti kwa mara ya kwanza shuleni wa kidato cha kwanza,awali na darasa la kwanza wakati wazazi wakiendelea kuwaandalia mazingira rafiki ya kuendelea masomo"ameeleza DC Pia amesema kuwa ofisi yake itahakikisha inafanya ufuatiliaji ndani ya wiki mbili ili kuhakikisha wanafunzi wote wanaopaswa kwenda shule waende kwa asilimia 100. Sima ameyasema hayo leo Januari 13,2025 wakati akitoa takwimu ya wanafunzi wanaopaswa kuanza kidato cha kwanza, darasa la kwanza na awali ambao tayari wamechukua fomu na wengine kujisajiri kwa ajili ya kuanza shule katika muhula wa kwanza kw...

Mkandarasi Ongeza Kasi ya Ujenzi Barabara ya Lusahunga-Rusumo

 Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya amemtaka Mkandarasi M/S China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) kuongeza kasi ya ujenzi wa barabara ya Lusahunga-Rusumo (km 92) kwa kiwango cha lami. Mhandisi Kasekenya ametoa agizo hilo tarehe 13 Januari 2025, Mkoani Kagera wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo ambapo ameridhishwa na hatua za ujenzi wa mradi huo. “Kazi inaonekana imeanza vizuri, hivyo Mhandisi Msimamizi uhakikishe unamsimamia Mkandarasi kwa ukaribu kwa kuongeza mitambo, wafanyakazi  na kuongeza masaa ya kazi ili kazi iweze kukamilika kwa muda uliopangwa”, amesema Mhandisi Kasekenya. Ameongeza kuwa Mkandarasi CCECC ni kampuni kubwa inayoaminiwa na Serikali kwenye suala zima la ufanisi wa kazi kwani wanafanyakazi nzuri na kazi kubwa wakisimamiwa vizuri. Aidha, amesema barabara ya Lusahunga-Rusumo ni kati ya barabara kubwa ambayo inategemewa katika uchumi wa Taifa kwani inaunganisha Tanzania na Nchi jirani za Rwanda, Burundi na D...

Rais Samia akutana na uongozi wa NMB Ikulu Dar es Salaam

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Tanzania Bi. Ruth Zaipuna Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Januari, 2025.

Rais Samia akutana na uongozi wa NMB Ikulu Dar es salaam

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Tanzania Bi. Ruth Zaipuna Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 13 Januari, 2025.