Skip to main content

Posts

Showing posts from September 16, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kutana na Maajabu ya Mchanga Unaooshwa Tanga

☑️ Watumika kwenye ujenzi wa miradi mikubwa kama Bandari ya Tanga, Bomba la Mafuta EACOP 📍 Tanga, Tanzania Sekta ya Madini nchini inaendelea kushuhudia mageuzi ya kuongeza thamani madini yakiwemo ya ujenzi kama mchanga na kufungua fursa nyingine mpya kwa wachimbaji wadogo wa mchanga kupitia teknolojia bunifu za usindikaji.  Katika mkoa wa Tanga, Kampuni ya Muwa Trading Tanzania Limited imewekeza kwenye Kiwanda cha kuosha na kusafisha mchanga kwa maji ili kuondoa udongo na uchafu mwingine kama mizizi, hatua ambayo imebadilisha kabisa mtazamo wa thamani ya rasilimali hiyo kwa miaka mingi. Kwa mkoa wa Tanga, unaojulikana kwa utajiri wa madini ya viwandani na ujenzi, mchanga safi unaopatikana baada ya kuoshwa sasa ni malighafi yenye thamani kubwa kwa viwanda vya saruji, miradi ya kimkakati ya Serikali ikiwemo Bandari ya Tanga na ujenzi wa Bomba la Mafuta la EACOP katika Kata ya Chongeleani.  Teknolojia hiyo pia inaelezwa kutoa fursa kwa wachimbaji wadogo na wawekezaji kuongeza ma...

Gavana wa Kisiwa cha Moheli aalika Wawekezaji toka Tanzania

Gavana wa Kisiwa cha Moheli nchini  Comoro,Mheshimiwa Chamina Ben Mohamed ametoa wito kwa wawekezaji wa sekta ya Utalii nchini Tanzania kutembelea kisiwa hicho kutathmini fursa katika eneo hilo ikiwemo ujenzi na uendeshaji wa hoteli na pia kuendesha kampuni za kuongoza watalii. Mheshimiwa Chamina ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Comoro,Saidi Yakubu ambaye yupo kisiwani humo kwa ziara ya kujitambulisha kwa wadau mbali mbali. “Kisiwa cha Moheli kina fukwe nzuri kujenga hoteli na kina vivutio zaidi vya Utalii kuliko kisiwa chochote kingine hapa Comoro na natambua Tanzania ina wadau wengi wa kushirikiana nasi,tunawakaribisha” alisema Gavana Chamine. Kwa upande wake,Balozi Yakubu alimueleza Gavana huyo kuwa Sekta ya Utalii ni miongoni mwa sekta zilizopiga hatua kubwa nchini Tanzania na atafikisha ujumbe huo kwa wadau husika. Aidha,Balozi Yakubu alipongeza pia juhudi za Serikali Kuu ya Comoro na Serikali ya Kisiwa hicho katika kuboresha miundombinu ya usa...

Pigeni Kura Oktoba 29, Mtudai Maendeleo - Dkt. Biteko

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukombe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Doto Mashaka Biteko amewaeleza wananchi wa Bukombe kuwa maendeleo yaliyopatikana jimboni humo yametokana na upendo wa Rais Samia Suluhu Hassan kwao, hivyo wajitokeze kuwapigia kura wagombea wa CCM ifikapo Oktoba 29 mwaka huu ili waendelee kupata maendeleo. Dkt. Biteko amesema hayo Septemba 16, 2025 katika mkutano wa kampeni uliofanyika Kata ya Runzewe Magharibi wilayani Bukombe mkoani Geita ikiwa ni sehemu Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu. Amesema katika kipindi cha miaka mitano ya Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan chini ya CCM imefanya kazi kubwa ya kuleta miradi ya maendeleo katika Kata hiyo ambayo miundombinu yake imefunguka zikiwemo ujenzi wa barabara, shule, miradi ya maji. Ameutaja  mradi wa Msasa ambao upo mbioni kupanuliwa ili kuhudumia wananchi wengi zaidi. Ameongeza kuwa katika kipindi hicho wamejenga Ofisi mpya ya Halmashauri...

Wajasiriamali Waliomba Dawati Maalum la Uwezeshaji la Tra Kuondoa Vikwazo

Na  Jovina Massano- Musoma. WAJASIRIAMALI mkoani Mara waiomba Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA)  kuhakikisha wanatatua na kusikiliza kero pamoja na changamoto zao kupitia dawati maalum la uwezeshaji lililoanzishwa ili kushiriki kikamilifu katika ulipaji mapato. Wameyasema hayo wakati wa hafla ya uzinduzi wa dawati maalum la uwezeshaji lilozinduliwa na mkuu wa mkoa wa Mara Kanali  Evans Mtambi katika viwanja vya TRA Manispaa ya Musoma Septemba 12, 2025. Uzinduzi huo ni utekelezaji wa mpango mkakati rafiki wa Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wafanyabiashara hapa nchini kuhakikisha kila mfanyabiashara anapata uelewa mpana wa umuhimu na wajibu wa kulipa kodi kwa maendeleo ya Taifa na kuendelea kuimarisha sekta ya biashara nchini ambapo  Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda, alilizindua kitaifa Agosti 16, 2025, mkoani Morogoro. Akiongea kwa niaba ya wafanyabiashara waliofika katika hafla hiyo Mwenyekiti ...

Dkt.Nchimbi Achanja Mbuga Kuzisaka Kura za Ushindi wa Kishindo wa Ccm Tanga

Mgombea Mwenza wa kiti cha Urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel  John Nchimbi leo Jumanne Septemba 16,2025 ameendelea na mikutano yake ya Kampeni za kusaka kura za ushindi akianzia kufanya mkutano katika viwanja vya Bokwa Wilaya ya Kilindi,na baadae akaelekea wilaya ya Muheza na kuwahutubia Wananchi katika uwanja wa Jitegemee,mkoani Tanga. Akiwa katika mikutano hiyo ya kampeni,Dkt.Nchimbi ambae ni Mgombea Mwenza wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan,pia alitumia nafasi hiyo ya kuwanadi Wagombea Ubunge na Madiwani wa mkoa huo. Dkt. Nchimbi anahitimisha kampeni zake leo ndani ya wilaya ya Mkinga Mkoa wa Tanga  huku akinadi Sera na Ilani ya chama hicho 2025-2030 kwa Wananchi, ikiwa ni katika harakati za kuomba ridhaa ya Watanzania  kuwaongoza katika awamu nyingine ya miaka mitano, katika Uchaguzi mkuu unaotarajiwa Kufanyika Oktoba 29, 2025

Pongezi Kwa Ghati Chomete

Mara.  Wananchi wa Mkoa wa Mara wanatoa pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Ghati Chomete,Mbunge wa Viti Maalum, kwa uongozi wake thabiti, ushujaa wa kisiasa, na moyo wa kujitoa kuwatumikia wananchi – hasa wanawake wa Mkoa wa Mara. Mheshimiwa Ghati Chomete ameendelea kuwa mstari wa mbele katika kutafuta kura za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan,kuwasemea wanawake wa Mkoa wa Mara na kuhakikisha kuwa sauti ya wanawake inasikika kwa nguvu katika majukwaa ya kisiasa. Kupitia ziara zake, mikutano ya hadhara na vikao na makundi mbalimbali ya kijamii, ameendelea kusambaza ujumbe wa matumaini, umoja na ushindi kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na wagombea wake wote. Uongozi wake umechochea ushiriki mpana wa wanawake kwenye siasa, ujasiriamali na maendeleo ya jamii kwa ujumla, na amekuwa daraja muhimu kati ya serikali na wananchi. Kwa hakika, *Mheshimiwa Ghati Chomete* umeonesha mfano wa kuigwa kwa wanawake viongozi—mshindi wa mioyo ya wananchi kwa unyenyekevu, ushawishi na utendaji....