Machi 07, 2026 *Mkuu wa Majeshi asema: Hakuna jambo la fidia *Aibua nderemo, shangwe kwa wananchi WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba ametoa majibu ya mgogoro wa ardhi baina ya wakazi wa Wilaya ya Monduli na Jeshi la Wananchi ambao wamedumu tangu 2004 baada ya kumpigia simu Mkuu wa Majeshi nchini na kumweleza kilio cha wanaMonduli. Waziri Mkuu alichukua hatua hiyo jana jioni (Ijumaa, Machi 6, 2026) wakati. na wananchi na viongozi mbalimbali kwenye mkutano wa hadhara ambao katika uwanja wa Barafu Mto wa Mbu, wilayani Monduli, mkoani Arusha. Akitoa majibu baada ya maongezi yao, Dkt. Mwigulueleza wananchi hao kwamba Mkuu wa Majeshi nchini ameridhia hoja yao ndiyo Mbunge wa Monduli, Isack Joseph pamoja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Namelok Sokoine ambao waliomba suala la fidia lisiwepo bali wananchi waachiwe kuendelea na jeshi kama ilivyokuwa zamani. “Mkuu wa Majeshi ameridhia kwamba hakuna jambo la fidia. Makubaliano mliyokuwa nayo awali ya mafunzo na malisho yaendelee vilevile....
Marato tv - Sauti ya Jamii