Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametangaza kuwa Jumatano, Juni 17, 2026, itakuwa siku rasmi ya mapumziko Zanzibar kwa ajili ya kuukaribisha Mwaka Mpya wa Kiislamu wa 1448 Hijria. Akitoa tamko hilo leo Ikulu Zanzibar, Rais Dkt. Mwinyi amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa uamuzi wa Serikali wa kuutambua Mwaka Mpya wa Kiislamu kama miongoni mwa siku muhimu zinazoadhimishwa Zanzibar. Amesema siku hiyo itawapa wananchi, hususan waumini wa dini ya Kiislamu, fursa ya kuukaribisha mwaka mpya kwa ibada, dua na matendo mema, pamoja na kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kuijaalia Zanzibar na Tanzania kwa ujumla amani, umoja na ustawi. Rais Dkt. Mwinyi amewahimiza wananchi kuutumia mwaka mpya wa Hijria kama kipindi cha kujitafakari, kuimarisha uchamungu, kusaidiana na kudumisha maadili mema yanayochangia kujenga jamii yenye mshikamano na maendeleo. Aidha, amezitaka taasisi za Serikali, taasisi binafsi, waajiri na wananchi wote kuzingatia tan...
Marato tv - Sauti ya Jamii