Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga ameahidi kuendeleza ushirikiano baina ya serikali na wenye viwanda kuhakikisha anatimiza ndoto za Rais Samia Suluhu Hassan za kuongeza idadi ya viwanda nchini. Aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wanachama na viongozi wa Shirikisho la Wenye Viwanda nchini (CTI), alipowatembelea kwenye ofisi zao jijini Dar es Salaam kujua changamoto zinazowakabili na kuweka mikakati kuzitatua. Alisema CTI ni wadau wakubwa kwenye maendeleo ya viwanda na ndiyo sababu ameamua kuwatembelea siku za mwanzo baada ya kuingia ofisi akiwa Waziri wa Viwanda. Alisema ameamua kuanza kutembelea shirikisho hilo kwa kuwa ni muhimu sana kwenye ustawi wa viwanda na linawafikia wadau 18,000 wa sekta hiyo ya viwanda. Waziri Kapinga alisema maono ya serikali ya awamu ya sita ni kuboresha uchumi wa viwanda kukuza ajira na kuendeleza kustawisha biashara na kukuza viwanda vya ndani. “Tumezungumza mengi na wenye viwanda na moja kubwa ...
Marato tv - Sauti ya Jamii