Skip to main content

Posts

Showing posts from May 24, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Soko La Kisasa la Nyama Choma Lazinduliwa Vingunguti

  Na John Mapepele Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe.Mohamed Mchengerwa   amezindua soko la kisasa la nyama choma la Kumbilamoto vingunguti, Ilala jijini Dar es Salaam na kushuhudia utiaji wa mikataba ya  miradi 6 ya maendeleo  yenye  thamani ya  shilingi bilioni 7.7 Mara baada ya kuzindua soko hilo ambalo limegharimu takribani shilingi milioni 727 amepongeza uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kufanikisha mradi huo ambapo amezitaka Halmashauri nyingine kuiga  mfano huo. Aidha, amefafanua kuwa soko hilo litakwenda kuwapatia ajira  wananchi wengi huku akisisitiza  kuendelea kulitunza  ili lisiharibike kwenye kipindi kifupi. Mhe. Mchengerwa ameongeza kuwa kukamilika kwa soko hilo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na  kufafanua kuwa Serikali ya awamu ya sita tayari imekamilisha  miradi  mingi kama iilivyoahidi. Wakati  huo huo Waziri Mchengerwa amezitaka Halmasha...

Mafanikio ya Sekta ya Madini katika Kipindi cha Miaka Minne ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan

*Dondoo za Aliyoyasema Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde katika Mkutano na Wahariri wa Vyombo vya Habari, Mei 24, 2025 Jijini Dar es Salaam.* *Mada: Mafanikio ya Sekta ya Madini katika Kipindi cha Miaka Minne ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan* 1. Ongezeko la Bajeti – Bajeti ya Wizara ya Madini imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Kutoka shilingi bilioni 89 mwaka wa fedha 2023/2024 hadi shilingi bilioni 231 kwa mwaka 2024/2025. Kwa mwaka ujao wa fedha 2025/2026, tumeidhinishiwa bajeti ya shilingi bilioni 224. Asilimia kubwa ya bajeti hii inaelekezwa kwenye Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kwa ajili ya kufanya tafiti za kina za jiolojia na ujenzi wa maabara ya kisasa ya uchambuzi wa madini katika eneo la Kizota, Dodoma. Lengo ni kuifanya GST kuwa kitovu cha huduma za maabara ya madini kwa Afrika nzima. Pia, maabara nyingine zinajengwa katika mikoa ya Geita na Chunya (Mbeya) ili kuboresha huduma za uchambuzi wa madini nchini. 2. Ongezeko la GDP –...

MRPC Yaadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo Vya Habari

 Na Ada Ouko, Tarime. CHAMA cha waandishi wa habari mkoa wa Mara(MRPC), Kimefanya Maadhimisho ya siku wa Uhuru wa vyombo vya habari mei 23 mwaka 2025, Kwa kuzingatia kauli mbiu ya mwaka huu kwa lengo la maendeleo ya tasnia ya habari. Akifungua maadhimisho hayo, mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Tarime Meja Edward Gowele alitoa wito kwa waandishi hao kuwa wazalendo, kwa kutathmini kazi zao, huku akiweka mkazo juu ya uweledi na ufanisi wa kalamu wanazotumia kuwa zinaweza kujenga au kubomoa jamii. "Tunataka maendeleo makubwa ya vyombo vya habari, kwa hiyo tuitumie hii siku kujitafakari fanyeni tathmini ya kazi zenu kwa mwaka uliopita ili kubaini mapungufu na changamoto ili kwamba muweze kuongeza ufanisi wa kazi zenu" alisema Gowele Mwenyekiti wa chama hicho Jacob Mugini, amesema kuwa kauli mbiu hiyo kwa lugha ya kingereza "The impact of artificial intelligence on press freedom and media"kwa maana ya Mchango wa akili Mnemba kwa Uhuru wa vyombo vya habari, wakiwemo waandis...

Balozi Nchimbi Aongoza Wajumbe wa Sekreterieti Kukagua Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Ccm

  Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akiambatana na Wajumbe wa Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa (NEC), leo Jumamosi, tarehe 24 Mei 2025, amekagua Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Convention Centre, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa CCM Taifa, utakaofanyika tarehe 29 na 30 Mei 2025, jijini Dodoma.

Makamu Wa Rais Aelezea Mikakati ya Kukabiliana na Janga la Njaa

 Na Ada Ouko -GMTV  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema ili kudhibiti janga la njaa na umasikini pamoja na kuharakisha maendeleo ya vijijini, ni vema mataifa kushirikiana kwa pamoja kwa kuwa masuala hayo ni janga la linalovuka mipaka ya nchi. Makamu wa Rais ametoa wito huo alipokuwa akitoa hotuba wakati wa majadiliano kuhusu “Muungano wa Kimataifa Dhidi ya Njaa na Sera za Umma kwa Usalama wa Chakula” katika Mkutano wa pili wa Brazil na Afrika kuhusu Usalama wa Chakula, Mapambano dhidi ya Njaa na Maendeleo Vijijini uliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Brazil (Itamaraty Palace) Jijini Brasilia. Amesema madhara ya umasikini na njaa ni makubwa sana na yameathiri zaidi bara la Afrika licha ya uwepo wa rasilimali za kutosha. Amempongeza Rais wa Brazil Mhe. Luiz Inácio Lula da Silva kwa juhudi alizozianzisha kuunganisha mataifa na kuhamasisha ushirikiano huo, kujidhatiti baina ya mataifa tajir...

Dkt. Biteko Awataka Wazazi Kuvumiliana Kutunza Familia Zao

  📌 Asisitiza wazazi kutenga muda wa kuwa na watoto wao 📌 Asema familia imara ni msingi wa dunia imara 📌 Mashirika, Wadau wa Maendeleo waipongeza Serikali kuimarisha malezi ya watoto 📌 Zaidi ya kaya 15,000 zapata elimu ya malezi jumuishi na huduma za afya ngazi ya jamii Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa rai kwa wazazi nchini kuvumiliana na kushirikiana katika malezi ya watoto wao ambao ndio msingi wa familia yeyote na Taifa kwa ujumla.  Dkt. Biteko ametoa rai hiyo Mei 24, 2025 jijini Mwanza wakati akimwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdory Mpango katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Familia yenye Kaulimbiu inayosema “ Mtoto ni Malezi: Msingi wa Familia Bora kwa Taifa Imara” “ Mtoto ni zao la matokeo ya wazazi wawili, Naomba wazazi tuthamini kuwa mtoto ni mtu muhimu na anahitaji  kulelewa, jambo hili la kutolea watoto likiendelea tut...