▪️Ampongeza Rais Samia kwa kuboresha mazingira ya Biashara nchini ▪️Wavutiwa na uwepo wa Rasilimali madini za kutosha ▪️Finland yaiahidi Tanzania ushirikiano kwenye utafiti wa madini 📍 Dar es Salaam Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde amewakaribisha jumuiya ya wa Wafanyabiashara kutoka Nchini Finland kuwekeza kwenye sekta ya madini kwa kuwa nchi ya Tanzania imejaaliwa kuwa na rasilimali ya kutosha ya madini,mazingira ya uwekezaji rafiki na sera zinazotabirika. Waziri Mavunde ameyasema hayo jana Masaki Jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa kifungua kinywa ulioandaliwa na Ubalozi wa Finland nchini kwa lengo la kuwakutanisha wafanyabiashara wa Madini kutoka Finland na Wizara ya Madini ili kubaini maeneo ya ushirikiano na fursa za kiuchumi zilizopo sekta ya madini nchini Tanzania. Akizungumza katika hafla hiyo Balozi wa Finland nchini Tanzania Mh. Theresa Zitting amesema Tanzania na Finland ni nchi zenye ushirikiano mkubwa kwenye masuala ya kiuchumi na hivyo ni wakatinmuafaka sa...
Marato tv - Sauti ya Jamii