Na Mwandishi Wetu, Ruvuma Serikali imesema utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la Mwaka 2023 juu elimu ya lazima kuwa ya miaka 10 utaanza Mwaka 2027/28 ambapo wahitimu wa elimu ya msingi ya miaka 6 watakutana na wahitimu wa mwisho wa elimu ya msingi ya miaka saba na wataanza kidato cha kwanza kwa pamoja. Hayo yameelezwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda Mkoani Ruvuma jana wakati akiwasilisha mada juu ya Sera Mpya ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo 2023 kwa wajumbe wa Baraza Kuu la Umoj wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi, Wenyeviti na Makatibu wa Wilaya (UWT) ambapo alisisitiza kuwa ifikapo Mwaka 2027/28 Mtoto ambaye hatakaa shuleni kwa miaka 10 hatua za kisheria zitachukuliwa kwa mzazi au mlezi. Waziri Mkenda ameongeza kuwa ili kuhakikisha utekelezaji wa sera mpya unakwenda sawa bila kikwazo chochote, Serikali inaendelea na kufanya mapitio ya Sharia ya Elimu, Sura ya 353 ili iendane na mabadiliko yali...
Marato tv - Sauti ya Jamii