Mbunge wa Jimbo la Butiama, Dkt. Charles Mahera, ameunga mkono kwa asilimia 100 Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2026/2027, akiieleza kuwa ni bajeti ya maendeleo iliyolenga kukuza uchumi, kuongeza mapato ya ndani, kuimarisha huduma za jamii na kuwezesha makundi mbalimbali ya wananchi kiuchumi. Akichangia Bajeti Kuu ya Serikali leo Bungeni jijini Dodoma, Dkt. Mahera alimpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake, pamoja na Waziri wa Fedha na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji kwa kuwasilisha bajeti aliyoieleza kuwa ya kimkakati na yenye kuzingatia mahitaji ya wananchi. Katika mchango wake, Dkt. Mahera ameipongeza Serikali kwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuwawezesha vijana, wanawake, wazee na wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga, akisema kundi hilo limeendelea kuwa mhimili muhimu wa uchumi wa wananchi. Ameishauri Serikali kuendelea kuboresha mazingira ya biashara kwa machinga kwa kuwapatia maeneo rasmi ya kufanyia biashara, ...
Marato tv - Sauti ya Jamii