Na OWM - TAMISEMI, Geita Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuidhinisha Shilingi 1,035,047,200/= za ujenzi wa dharura wa barabara ya Kasamwa- Gamashi yenye urefu wa kilomita 18, iliyoimarisha shughuli za kiuchumi kupitia Sekta ya Usafiri na Usafirishaji kati ya Wilaya ya Nyang’hwale na Makao Makuu ya Mkoa wa Geita. Prof. Shemdoe amesema barabara hiyo ina umuhimu kiuchumi kwa wananchi wa Nyang’hwale na Geita ambao wanategemea shughuli za kilimo na ufugaji, hivyo uzalishaji unaofanyika Nyang’hwale ulikuwa hauwezi kufika makao makuu ya mkoa kutokana na changamoto iliyokuwepo ya ubovu wa miundombinu ya barabara ya Kasamwa- Gamashi. “Ujenzi wa barabara hii ni muhimu sana kiuchumi, hivyo tunapaswa kumshukuru Mhe. Rais kwa kuidhinisha fedha zilizowezesha barabara kujengwa ili kuendeleza shughuli za wananchi kiuchumi,” amesisitiza Prof. Shemdoe. Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amempongeza Mshauri...
Marato tv - Sauti ya Jamii